Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Lakini kama hamutanisikiliza wala kufuata amri zangu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:14
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Mwende muombe shauri kutoka kwa Yawe kwa ajili yangu, na kwa watu wa Yuda wote juu ya maneno ya kitabu hiki kilichopatikana kwa sababu kasirani ya Yawe imewaka juu yetu, maana babu zetu hawakutii maneno ya kitabu hiki na kutimiza yote yaliyoandikwa juu yetu.”


Yawe anasema hivi: ‘Angalia nitaleta uovu juu ya Yerusalema na juu ya wakaaji wake, laana zote zilizoandikwa katika kitabu kilichosomwa mbele ya mufalme wa Yuda.


“Lakini mukiacha kunifuata, na kuasi maongozi yangu na amri nilizowapa, na kwenda kutumikia miungu mingine na kuiabudu,


“Lakini watu wangu hawakunisikiliza; Israeli hakunitaka kabisa.


Yawe analaani nyumba za waovu, lakini anabariki makao ya wenye haki.


Lakini wao hawakunitii, wala hawakunisikiliza. Kila mumoja wao alizidi kuwa mugumu na mwovu. Basi, niliwaazibu kulingana na masharti ya agano hili nililowaamuru kushika, lakini hao wakakataa kulishika.


Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika. –Ni ujumbe wa Yawe.


Utawaambia kwamba: Yawe anasema hivi: Kama hamutanisikiliza na kufuata sheria zangu nilizowawekea,


Manabii waliotangulia mbele yetu, mimi na wewe, zamani za kale walitabiri kwamba vita, njaa na magonjwa makali vitazipata inchi nyingi na tawala kubwa.


Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.


Mukubwa wa walinzi alimukamata Yeremia, akamwambia: Yawe, Mungu wako, alitangaza hasara juu ya pahali hapa.


Lakini Yawe amefanya sawa kwa maana nimeliasi neno lake. Munisikilize enyi watu wote, muyaangalie mateso yangu. Wabinti zangu na vijana wangu wanaume wamepelekwa katika utumwa.


Yawe amefanya yale aliyokusudia, ametimiza yale aliyoagiza. Kama alivyopanga tangu kale, ameangamiza bila huruma yoyote. Amewafanya waadui wafurahie azabu yako, amewatukuza mashujaa wa waadui zako.


Umetuazibu kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, lakini mpaka sasa, ee Yawe, Mungu wetu, hatukuomba musamaha wako kwa kuziacha zambi zetu na kutambua uaminifu wako.


Watakapokwenda nitatandaza wavu wangu niwanase, nitawaangusha chini kama ndege toka katika anga; nitamwaazibu kufuatana na jinsi walivyotangaza kwa kusanyiko lao.


Na kama hata kisha kuazibiwa hivyo hamutanisikiliza, basi, nitawaazibu mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


Ni lazima muniheshimu mimi kwa matendo yenu. Musiponisikiliza nitawaletea laana. Vitu vyote munavyopewa kwa mahitaji yenu nitavilaani. Na kweli nimekwisha kuvilaani, kwa sababu hamushuguliki hata kidogo na maagizo yangu.


Na mutu yeyote atakayekataa kumusikiliza nabii yule, atatengwa mbali na taifa la Mungu na kuuawa.’


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Lakini kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyotimiza mambo yote mema aliyowaahidi, ni vile vile anavyoweza kuwaletea maovu yote mpaka awaangamize wote kutoka inchi hii nzuri ambayo amewapa.


Kila mara walipokwenda kupigana, mukono wa Yawe ulipambana nao kwa kuwaletea hasara, kama alivyokuwa amewaonya na kuapa. Nao wakakuwa katika huzuni kubwa.


Lakini kama hamutasikiliza sauti ya Yawe, mukiasi amri yake, basi yeye atapambana nanyi pamoja na mufalme wenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ