Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi musikuwe watumwa wa Wamisri. Mimi nimevunja nira muliyofungiwa katika shingo lenu na kuwafanya mutembee wima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:13
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Yawe, mimi ni mutumishi wako, mutumishi wako, mutoto wa mujakazi wako. Umenifungulia vifungo vyangu.


Yawe akafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye akawafuatilia Waisraeli ambao walikuwa wameondoka Misri katika uhuru.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Nami nitakitia katika mikono ya wanaokutesa, waliokuambia ulalie tumbo wapite juu yako, nawe ukaufanya mugongo wako kama vile udongo wa njia, kama vile barabara ya kupitia.


Maana miti mizito waliyobeba, nira walizokuwa wamefungwa, na fimbo ya wasimamizi, umezivunjavunja kama wakati wa Wamidiani.


Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimevunja nira mufalme wa Babeli anayowabebesha.


Vilevile nitamurudisha Yekonia mwana wa Yoyakimu mufalme wa Yuda pamoja na watu wote wa Yuda waliohamishiwa Babeli. Hakika nitaivunja nira mufalme wa Babeli anayowabebesha. –Ni ujumbe wa Yawe.


Huko Tapanesi muchana utakuwa giza wakati nitakapovunja mamlaka ya Misri na kiburi chake kikubwa kitakapokomeshwa. Wingu litaifunika inchi ya Misri na watu wake watakamatwa mateka.


Miti inayokuwa katika mashamba itazaa matunda, udongo utatoa mazao kwa wingi, nao wataishi kwa salama katika inchi yao. Nitakapovunja nira zao za utumwa na kuwaokoa toka katika mikono ya hao waliowafanya kuwa watumwa halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Niliwaongoza kwa huruma, nilishikamana nao kwa upendo; kama baba anavyomunyanyua mutoto mpaka kwenye shavu lake, ndivyo nami nilivyokuwa kwao. Mimi niliinama chini na kuwakulisha.


Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyekutoa kutoka inchi ya Misri kwa kukupa inchi ya Kanana, na kusudi nami nikuwe Mungu wako.


Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu ambao niliwatoa katika inchi ya Misri, basi, wasiuzishwe kama watumwa.


Waisraeli ni watumishi wangu, maana niliwatoa katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Sasa nitaivunja nira ya Asuria katika shingo lenu, na minyororo waliyowafungia nitaikatakata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ