Kila pahali ambako nimekwenda na Waisraeli wote, sikumwuliza mwamuzi yeyote wa Israeli ambaye nilimwamuru awachunge watu wa Israeli: ‘Kwa nini haujanijengea nyumba ya mierezi?’
“Lakini, ee Mungu, kweli utakaa katika dunia? Ikiwa hata mbingu zenyewe wala mbingu za juu sana hazikutosha, namna gani nyumba hii ambayo nimeijenga itakutoshelea?
Yawe amechukia mazabahu yake na hekalu lake amelikataa. Amewaachilia waadui wazibomoe kuta za nyumba zake katika muji. Wakapiga kelele ndani ya nyumba ya Yawe kama kelele za wakati wa sikukuu.
Mutatambua kwamba mimi niko kati yenu, enyi Waisraeli; na kwamba mimi Yawe, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.
Wakati watakapokuwa inje ya inchi yao, inchi hiyo itafurahia Sabato zake hapo itakapokuwa katika hali ya ukiwa. Wakati huo wao watatubu uovu wao wa kuzarau maagizo yangu na kuchukia masharti yangu.
Basi, ikiwa inchi yenu muliorizi ni chafu, mukuje katika inchi ya Yawe ambako hema yake iko na kujitwalia sehemu kule pamoja nasi; lakini tu musimwasi Yawe na kutufanya sisi wote waasi kwa kujijengea ninyi wenyewe mazabahu isiyokuwa ya Yawe, Mungu wetu.
Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akayaambia makabila ya Rubeni na Gadi na nusu ya kabila la Manase: “Leo tumejua kwamba Yawe yuko kati yenu maana hamukumufanyia Mungu uasi. Sasa mumewaokoa Waisraeli wasiazibiwe na Yawe.”
Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.
Ndiyo maana wanasimama mbele ya kiti cha kifalme cha Mungu, nao wanamutumikia muchana na usiku katika hekalu lake. Na yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme atawalinda katika hema yake.