Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Musijitengenezee sanamu za miungu ya uongo, musishike sanamu zao za kuchongwa wala nguzo wala sanamu za mawe yaliyochongwa katika inchi yenu na kuviabudu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:1
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Juu ya kila kilima na chini ya kila muti wenye majani mabichi, walijenga nguzo za mawe na sanamu za miungu wa kike Ashera,


Walivunja amri zote za Yawe, Mungu wao. Wakatengeneza sanamu za miungu ya wana-ngombe wawili wa madini yenye kuyeyushwa, wakatengeneza sanamu za Ashera, wakaabudu jeshi la mbingu, na wakamutumikia Bali.


na kufuata njia za mataifa ambayo Yawe aliyafukuza wakati watu wake walipokuwa wanaingia, na kufanya matendo ya wafalme wa Israeli waliyoyaingiza katika inchi.


Walimukasirikisha kwa mazabahu zao za miungu; wakamutia wivu kwa sanamu zao za kuchongwa.


Wote wanaoabudu sanamu na kujisifia miungu ya bure wanafezeheshwa. Miungu yote inainama mbele yake.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Mutaniheshimu mimi peke yangu wala musijifanyie miungu ya feza wala ya zahabu.


Musiiname mbele ya miungu yao kuiabudu, wala kuitumikia, wala musiige mambo yao. Lakini mutawaangamiza kabisa na kuvunjavunja nguzo zao.


Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo sanamu za feza na zahabu walizojitengenezea kusudi waziabudu.


Musigeukie sanamu za miungu, wala musijitengenezee sanamu za kuyeyushwa za miungu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Waisraeli ni watumishi wangu, maana niliwatoa katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Muguu huo utakuwa mali ya kuhani anayekuwa muzao wa Haruni anayetolea damu ya sadaka za amani na mafuta yake.


muwafukuze wenyeji wote wa inchi hiyo mbele yenu. Mutaziharibu sanamu zao zote za mawe na za kuyeyushwa na kubomoa kila pahali pao pa ibada.


Basi kwa kuwa sisi tuko watoto wa Mungu, tusiwaze kwamba anafanana na sanamu ya zahabu au ya feza au ya jiwe, iliyochorwa kwa ufundi na akili ya watu.


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayefanya sanamu ya kuchonga au ya kuyeyushwa na kuisimamisha kwa siri, kitu ambacho kimetengenezwa na mikono ya fundi na ambacho ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


“Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Lakini mbali ya muji ule kuna watu wenye kuchukiza, wachawi, wazinzi, wauaji, wanaobudu sanamu na wasema uongo na wote wanaoupenda.


Watu wa kabila la Dani wakaisimika ile sanamu ya kuchonga, naye Yonatani mwana wa Gersoni, mujukuu wa Musa, akakuwa kuhani wao. Wazao wake vilevile walikuwa makuhani wa kabila la Dani mpaka wanainchi wa inchi hiyo walipopelekwa katika uhamisho.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ