Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 24:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mikate hiyo itapangwa kwa mistari miwili juu ya meza ya zahabu safi, kila mustari mikate sita.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 24:6
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Solomono alitengeneza vifaa vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Yawe: mazabahu ya zahabu meza kwa ajili ya mikate ya kuwekwa mbele ya Mungu –meza ile ilifunikwa na zahabu– vinara vya taa vilivyowekwa mbele ya Pahali Patakatifu Sana, vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini –vilifunikwa na zahabu safi– maua taa koleo –vilifunikwa na zahabu– vikombe makasi ya kukata tambi za mishumaa mabakuli vyetezo vya kuwekea ubani miko ya kuopoa moto –vilifunikwa na zahabu safi– vyuma vya kushika milango ya sehemu ya Pahali Patakatifu Sana vyuma vya kushika milango ya hekalu –vilifunikwa na zahabu.


Kila siku asubui na magaribi, makuhani wanamutolea sadaka za kuteketezwa na kumufukizia ubani wenye harufu nzuri, tena wanapanga mikate inayotolewa na Mungu juu ya meza ya zahabu safi, na kutunza kinara cha zahabu na kuwasha taa kila siku magaribi. Sisi tunayafuata maagizo ya Yawe, Mungu wetu, lakini ninyi mumemwacha.


Solomono alitengeneza vitu vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Mungu: mazabahu ya zahabu na meza za mikate mitakatifu;


Tunajiwekea sheria juu yetu kwamba, kwa mwaka tutatoa sehemu moja ya tatu ya kikoroti kimoja cha feza kwa ajili ya kazi za nyumba ya Mungu:


kwa ajili ya mikate mitakatifu, sadaka za unga za kawaida, sadaka za kuteketezwa kwa moto za kawaida, sadaka za siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, sikukuu nyingine zilizowekwa, vitu vingine vitakatifu, sadaka za kusamehewa zambi, kwa kuwafanyia upatanisho watu wa Israeli na kazi nyingine zozote za nyumba ya Mungu wetu.


Meza hiyo utaiweka mbele ya Sanduku la Agano na juu ya meza ile utaweka ile mikate muliyonitolea. Mikate ile itakuwa siku zote mbele yangu.


meza na vyombo vyake vyote, mikate iliyotolewa kwa Mungu;


mazabahu ya mbao. Urefu wake kwenda juu ulikuwa metre moja na nusu na upana wa metre moja. Pembe zake, tako lake, na pande zake zote zilikuwa zimetengenezwa kwa mbao. Yule mutu akaniambia hivi: Hii ndiyo meza inayokaa mbele ya Yawe.


Lakini maneno yote yatendeke katika usawa na katika utaratibu.


Kufuatana na ile, kulikuwa Hema iliyosimikwa. Chumba chake cha kwanza kiliitwa Pahali Patakatifu. Ndani ya chumba kile kulikuwa kinara cha kuwekea taa, meza na mikate iliyotolewa kwa Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ