Solomono alitengeneza vifaa vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Yawe: mazabahu ya zahabu meza kwa ajili ya mikate ya kuwekwa mbele ya Mungu –meza ile ilifunikwa na zahabu– vinara vya taa vilivyowekwa mbele ya Pahali Patakatifu Sana, vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini –vilifunikwa na zahabu safi– maua taa koleo –vilifunikwa na zahabu– vikombe makasi ya kukata tambi za mishumaa mabakuli vyetezo vya kuwekea ubani miko ya kuopoa moto –vilifunikwa na zahabu safi– vyuma vya kushika milango ya sehemu ya Pahali Patakatifu Sana vyuma vya kushika milango ya hekalu –vilifunikwa na zahabu.