Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 24:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Twaa unga laini, kilo kumi na mbili na kupika mikate kumi na miwili.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 24:5
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alitwaa mawe kumi na mawili, hesabu ya makabila kumi na mawili yaliyopewa majina ya wana wa Yakobo ambaye neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Jina lako litakuwa Israeli.”


Pamoja na hayo, walisaidia katika kazi kutayarisha mikate mitakatifu, unga safi na sadaka ya vyakula, maandazi yasiyotiwa chachu, sadaka ya mikate iliyokaangwa, sadaka ya mikate iliyochanganywa na mafuta, na sadaka katika kazi ya upimaji wa wingi wa sadaka na ukubwa wake.


Nao wandugu zao wengine wa ukoo wa Kohati walikuwa na kazi ya kutayarisha mikate iliyotolewa kwa Mungu kila siku ya Sabato.


Kila siku asubui na magaribi, makuhani wanamutolea sadaka za kuteketezwa na kumufukizia ubani wenye harufu nzuri, tena wanapanga mikate inayotolewa na Mungu juu ya meza ya zahabu safi, na kutunza kinara cha zahabu na kuwasha taa kila siku magaribi. Sisi tunayafuata maagizo ya Yawe, Mungu wetu, lakini ninyi mumemwacha.


Tunajiwekea sheria juu yetu kwamba, kwa mwaka tutatoa sehemu moja ya tatu ya kikoroti kimoja cha feza kwa ajili ya kazi za nyumba ya Mungu:


kwa ajili ya mikate mitakatifu, sadaka za unga za kawaida, sadaka za kuteketezwa kwa moto za kawaida, sadaka za siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, sikukuu nyingine zilizowekwa, vitu vingine vitakatifu, sadaka za kusamehewa zambi, kwa kuwafanyia upatanisho watu wa Israeli na kazi nyingine zozote za nyumba ya Mungu wetu.


Meza hiyo utaiweka mbele ya Sanduku la Agano na juu ya meza ile utaweka ile mikate muliyonitolea. Mikate ile itakuwa siku zote mbele yangu.


meza na vyombo vyake vyote, mikate iliyotolewa kwa Mungu;


na juu yake akapanga mikate iliyotolewa kwa Yawe, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Utaingiza meza na kupanga vyombo vyake juu. Utaingiza kile kinara vilevile na kuweka taa zake juu yake.


Juu ya meza ya kutolea mikate inayowekwa mbele ya Yawe watatandaza kitambaa cha rangi ya samawi na juu yake wataweka sahani, visahani vya ubani, bakuli na bilauri, kwa ajili ya kutolea sadaka za kinywaji. Siku zote kutakuwa mukate juu ya meza.


Aliingia ndani ya nyumba ya Mungu na kula mikate mitakatifu iliyotolewa kwa Mungu. Ijapokuwa vile haikuruhusiwa kwake wala kwa watu wake kukula mikate kama ile, isipokuwa makuhani peke yao.


Makabila yetu kumi na mawili wanamwabudu Mungu usiku na muchana, kwa maana wanatumaini kuona utimilifu wa ile ahadi. Na ni kwa sababu ya tumaini lile, Ee mufalme, Wayuda wananishitaki.


Kufuatana na ile, kulikuwa Hema iliyosimikwa. Chumba chake cha kwanza kiliitwa Pahali Patakatifu. Ndani ya chumba kile kulikuwa kinara cha kuwekea taa, meza na mikate iliyotolewa kwa Mungu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yakobo, mutumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. Ninawasalimia ninyi watu wa makabila kumi na mawili waliosambazwa katika dunia.


Daudi akamwambia: “Kwa hakika, ninapokwenda kwa ajili ya shuguli kubwa, wanawake wanatengwa mbali nasi! Ikiwa miili ya vijana wangu inakuwa mitakatifu na safi tunapokuwa kwenye shuguli za kawaida, basi, si zaidi katika shuguli hii kubwa?”


Kwa hiyo kuhani Ahimeleki akamupa mikate mitakatifu, maana hapakukuwa mikate mingine isipokuwa ile ambayo inaondolewa mbele ya Yawe na kubadilishwa na mikate mipya kutoka kwenye jiko.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ