Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 24:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Sheria hii inaelekea mugeni na mwenyeji. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 24:22
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sheria zilezile zitaelekea Mwisraeli aliyezaliwa katika inchi na wageni watakaoishi kati yenu.”


Kama mutu yeyote wa jamii ya Israeli au mugeni anayeishi kati yao anakula damu yoyote, mimi nitamukasirikia mutu yule aliyekula damu na kumutenga mbali na watu wake.


Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Basi, Musa akawaambia Waisraeli hayo yote. Wakamupeleka yule mutu aliyelaani Yawe inje ya kambi, wakamwua kwa kumupiga mawe. Ndivyo Waisraeli walivyofanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Mutafuata sheria moja kila mutu atakayekosa bila kukusudia, akuwe ni mwanainchi Mwisraeli au ni mugeni anayeishi pamoja nanyi.


Ikiwa kuna mugeni anayeishi pamoja nanyi na anapenda kufanya sikukuu ya Pasaka, mutu huyo sharti afanye hivyo kulingana na masharti na maagizo yote ya Pasaka. Kila mutu atafuata masharti yaleyale, akiwa mugeni au mwenyeji.


“Wakati uleule nikawapa waamuzi wenu maagizo haya: ‘Musikilize maneno ya watu wenu. Mutoe hukumu za haki katika maneno kati ya kila mumoja na ndugu yake au na wageni wanaoishi pamoja nanyi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ