Kama mutu yeyote wa jamii ya Israeli au mugeni anayeishi kati yao anakula damu yoyote, mimi nitamukasirikia mutu yule aliyekula damu na kumutenga mbali na watu wake.
Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Basi, Musa akawaambia Waisraeli hayo yote. Wakamupeleka yule mutu aliyelaani Yawe inje ya kambi, wakamwua kwa kumupiga mawe. Ndivyo Waisraeli walivyofanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Ikiwa kuna mugeni anayeishi pamoja nanyi na anapenda kufanya sikukuu ya Pasaka, mutu huyo sharti afanye hivyo kulingana na masharti na maagizo yote ya Pasaka. Kila mutu atafuata masharti yaleyale, akiwa mugeni au mwenyeji.
“Wakati uleule nikawapa waamuzi wenu maagizo haya: ‘Musikilize maneno ya watu wenu. Mutoe hukumu za haki katika maneno kati ya kila mumoja na ndugu yake au na wageni wanaoishi pamoja nanyi.