Walawi 24:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
14 Umuondoe kijana aliyetukana inje ya kambi, wale wote waliomusikia akitukana waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na wote pamoja wamwue kwa kumupiga mawe.
Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu yeyote kati ya Waisraeli au mugeni anayekaa kati yenu, akimutoa mutoto wake yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki, mutu huyu anapaswa kuuawa. Wanainchi wa pale watamwua kwa kumupiga mawe.
Hapo watu wa muji huo watamupiga mutoto huyo mawe mpaka akufe. Ndivyo mutakavyokomesha ubaya huo kati yenu. Kila mutu katika Israeli atasikia tukio hilo na kuogopa.
watamupeleka kwenye mulango wa nyumba ya baba yake na wanaume wa muji huo watamupiga mawe akufe, kwa sababu amefanya upumbafu katika Israeli kwa kufanya ukahaba akiwa katika nyumba ya baba yake. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.
Yoshua akamwuliza Akana: “Kwa nini umetuletea taabu? Yawe atakuletea taabu wewe mwenyewe leo.” Waisraeli wote wakamupiga Akana kwa mawe mpaka akakufa. Kisha wakawapiga jamaa yake yote kwa mawe mpaka wakakufa, wakawateketeza wote kwa moto.