Walawi 23:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 Kwa muda wa siku hizo zote saba mutanitolea mimi Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto. Katika siku ya saba mutafanya mukutano mutakatifu. Musifanye kazi.
Siku ya kwanza na siku ya saba mutakuwa na mukutano mutakatifu. Katika siku hizo mbili hamutaruhusiwa kufanya kazi yoyote isipokuwa kazi ya lazima ya kutayarisha chakula.
Kila siku, katika muda huo wa siku saba, atamutolea Yawe sadaka ya ngombe dume saba na kondoo dume saba wasiokuwa na kilema kwa kuwateketeza kwa moto. Tena ni lazima atoe sadaka kila siku kuwa sadaka ya kusamehewa zambi.
Katika siku sita mutakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya saba kutakuwa mukutano mukubwa wa kumwabudu Yawe, na hamutafanya kazi yoyote katika siku hiyo.