Siku ya kwanza na siku ya saba mutakuwa na mukutano mutakatifu. Katika siku hizo mbili hamutaruhusiwa kufanya kazi yoyote isipokuwa kazi ya lazima ya kutayarisha chakula.
Kwa muda wa siku hizo zote saba mutanitolea mimi Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto. Katika siku ya saba mutafanya mukutano mutakatifu. Musifanye kazi.