Hivyo wakatangaza katika miji yao yote na kule Yerusalema, wakisema: “Mwende kwenye milima, mulete matawi ya mizeituni, mizeituni ya pori, mihadasi, mingazi na miti mingine kwa kujenga vibanda, kama vile ilivyoandikwa.”
Hizo ndizo sikukuu za Yawe zilizopangwa ambazo mutatoa tangazo kuwe mukutano mutakatifu wa kumutolea Yawe sadaka zinazotolewa kwa moto, sadaka za kuteketezwa na sadaka za vyakula, matoleo na sadaka za kinywaji, kila moja kwa siku yake yenyewe.