Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 23:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Uwaambie Waisraeli hivi: Tangu siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba mutafanya sikukuu ya vibanda kwa muda wa siku saba kwa heshima ya Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 23:34
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeroboamu aliamuru vilevile siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane ikuwe sikukuu sawa na ile sikukuu iliyokuwa inafanyika kule Yuda. Alitoa sadaka kwenye mazabahu aliyotengeneza kule Beteli mbele ya zile sanamu za wana-ngombe alizozitengeneza, akaweka wale makuhani aliowachagua watumike kila nafasi ya kutolea sadaka aliyotengeneza juu ya vilima.


Halafu watu hao wote wakakusanyika mbele ya mufalme Solomono wakati wa sikukuu ya mwezi wa Etanimu, ni kusema mwezi wa saba.


Naye Solomono kwa muda wa siku saba alifanya sikukuu pamoja na Waisraeli wote. Nao walitoka tangu kwenye kiingilio cha Hamati, mpaka muto wa Misri.


Wakafanya sikukuu ya vibanda kama ilivyoandikwa katika Sheria; kila siku walitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizohitajika kwa ajili ya siku hiyo.


Wakagundua kwamba, imeandikwa katika kitabu cha Sheria kuwa Yawe alimwamuru Musa, kwamba watu wanapaswa kukaa katika vibanda wakati wa sikukuu ya mwezi wa saba.


Mutafanya sikukuu ya mavuno ya kwanza ya kazi zenu na ya mavuno ya mashamba yenu. Mutafanya sikukuu ya kukusanya mavuno mwisho wa mwaka munapokusanya mazao ya kazi zenu.


Mutashika sikukuu ya majuma kwa mwanzo wa wakati wa mavuno ya ngano na kufanya sikukuu ya kukusanya mavuno kwa mwisho wa mwaka.


Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, na kwa muda wa siku saba za sikukuu, mufalme atatoa mahitaji kwa ajili ya sadaka za kusamehewa zambi, sadaka za kuteketezwa kwa moto, sadaka za vyakula na mafuta.


Kwa muda wa siku saba mutaishi katika vibanda. Wakaaji wote wa Israeli wataishi katika vibanda wakati huo.


Jambo hilo litajulisha vizazi vyenu kwamba nilipowatoa babu zenu katika inchi ya Misri, niliwafanya waishi katika vibanda. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mutafanya mukutano mutakatifu. Hamutafanya kazi siku hiyo. Mutafanya sikukuu kwa ajili ya Yawe kwa siku saba.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Sikukuu moja ya Wayuda inayoitwa Sikukuu ya Vibanda ilipokuwa karibu,


“Wanaume wote wa taifa lenu watakuja mbele ya Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka, pahali ambapo Yawe, Mungu wenu atachagua: wakati wa sikukuu ya Pasaka, sikukuu ya kuvuna na wakati wa sikukuu ya vibanda. Wasitokee mbele ya Yawe mikono mitupu.


Kisha akawaamuru akasema: “Kila mwaka wa saba utakuwa mwaka wa mafungulio. Katika sikukuu ya vibanda, mwaka huo,


Watu hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea mambo Mungu aliyoahidi. Lakini waliyaona kwa mbali na kuyafurahia, wakikubali kwamba walikuwa wageni na wasafiri katika dunia.


Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ