Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 23:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Siku hiyo, itakuwa kwenu Sabato ya mapumziko na mutafunga. Siku ya Sabato ni siku ya kumi ya mwezi huo tangu magaribi mpaka magaribi inayofuata.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 23:32
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi tufanye bidii ya kuingia kwenye mapumziko yale, kusudi hata mutu mumoja asianguke sawa vile wale walioasi katika jangwa.


Lakini sasa sisi tulioamini, tutaingia kwenye mapumziko ambayo Mungu alitaja aliposema: “Halafu nikaapa kwa kasirani kwamba hawataingia hata kidogo kwenye mapumziko niliyowatayarishia!” Mungu alisema vile ingawa alikuwa amemaliza kazi zake tangu pale alipoumba dunia.


Lakini tungejichunguza sisi wenyewe kwanza, hatungehukumiwa na Mungu.


Heri wale wanaokuwa na huzuni, maana Mungu atawafariji!


na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Ee Bwana, uniwezeshe kusema, midomo yangu itangaze sifa zako.


Lakini wao walipokuwa wagonjwa, mimi nilivaa magunia kuonyesha huzuni, nilijitesa kwa kufunga kula chakula. Niliomba nikikuwa nimeinamisha kichwa.


Siku ya kumi ya mwezi huu wa saba ni siku ya upatanisho. Siku hiyo ni siku ya kuwa na mukutano mutakatifu. Mutafunga kula na kutoa sadaka Yawe anazotolewa kwa moto.


Siku hiyo ni siku ya mapumziko kamili nanyi mutafunga. Hili ni sharti la kufuata siku zote.


Musifanye kazi: hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu, na katika makao yenu yote.


Halafu, nikaamuru kwamba milango ya Yerusalema ifungwe wakati siku ya Sabato inapoanza magaribi, wakati giza linapoanza kuingia, na isifunguliwe mpaka Sabato imekwisha. Nikaweka watumishi wangu wamoja kwenye milango na kuwaagiza kwamba kitu chochote kisiletwe katika muji siku ya Sabato.


Hili ni sharti la kufuata siku zote: Siku ya kumi ya mwezi wa saba, ninyi wenyewe na hata wageni wanaoishi kati yenu, munapaswa kufunga kula siku hiyo na kuacha kufanya kazi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ