16 Katika siku ya makumi tano, siku ya pili ya Sabato ya saba, mutanitolea mimi Yawe sadaka ya vyakula vipya.
Katika mwezi wa tatu wakaanza kuvipanga katika mafungu, wakamaliza katika mwezi wa saba.
Kila jamaa italeta mikate miwili ya sadaka ya kutoa kwa kitambulisho mbele yangu mimi Yawe. Kila mukate utatengenezwa kwa kilo mbili za unga laini uliotiwa chachu na huo mutanitolea mimi Yawe ukiwa ni matoleo ya malimbuko yenu.
Katika siku ya kwanza ya sikukuu ya majuma wakati munapomutolea Yawe malimbuko ya ngano zenu, mutafanya mukutano mutakatifu; musifanye kazi.
Wakati siku ya Pentekoste ilipotimia, wanafunzi walikuwa wamekusanyika wote pamoja wakibaki kwenye nafasi moja.