Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 23:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mbele ya siku hiyo ya kuniletea mimi Mungu wenu sadaka hiyo, hamuruhusiwi kula mazao ya kwanza ya mavuno yenu, yakuwe mabichi, yamekaangwa au yemepikwa kuwa mikate. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu pahali popote mutakapoishi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 23:14
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mazao ya kwanza ya shamba yako utayaleta katika nyumba yangu mimi Yawe, Mungu wako. Usipike mwana-kondoo au mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.


Kwa njia ya Musa, mutumishi wako, ukawajulisha siku zako za Sabato takatifu na ukawaagiza kuzifuata amri, masharti na sheria ulizowaamuru.


Mukumbuke kwamba mulikuwa watumwa kule Misri na mukuwe waangalifu kufuata masharti haya.


Mutawafundisha Waisraeli masharti yote ambayo nimewaambia kwa njia ya Musa.


Ndiyo maana munapaswa kufuata sharti hili siku zote na pahali popote mutakapokaa. Musikule hata kidogo mafuta wala damu.


Sheria ya Yawe ni kamilifu; inamupa mutu uzima mupya. Maagizo ya Yawe ni ya kuaminiwa; yanawapa wajinga hekima.


Ukimutolea Yawe sadaka ya mazao yako ya kwanza utaitoa hiyo ikiwa imechomwa katika masuke yake, au utaitoa katika mikate ya kuchomwa iliyotengenezwa kwa ngano iliyosagwa.


Hiyo itakuwa ndani ya hema la mukutano inje ya pazia lile mbele ya Sanduku la Agano na Haruni na wana wake wataitunza mbele yangu tangu magaribi mpaka asubui. Sharti hili lifuatwe siku zote na Waisraeli wote, kizazi kwa kizazi.


Musifanye kazi: hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu, na katika makao yenu yote.


Kila mwaka munapaswa kufanya sikukuu hii kwa muda wa siku saba kwa heshima ya Yawe. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu. Mutaifanya katika mwezi wa saba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ