Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 23:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Uwaambie Waisraeli hivi: Mutakapoingia katika inchi ambayo ninawapa na kuvuna mazao yake, mutamuletea kuhani muganda wa mavuno ya kwanza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 23:10
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutafanya vile vile juu ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mutamwacha kila muzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba na siku ya nane mutanitolea.


Mutafanya sikukuu ya mavuno ya kwanza ya kazi zenu na ya mavuno ya mashamba yenu. Mutafanya sikukuu ya kukusanya mavuno mwisho wa mwaka munapokusanya mazao ya kazi zenu.


Mazao ya kwanza ya shamba lako utayaleta katika nyumba yangu mimi Yawe, Mungu wako. Usipike mwana-kondoo au mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.


Mutashika sikukuu ya majuma kwa mwanzo wa wakati wa mavuno ya ngano na kufanya sikukuu ya kukusanya mavuno kwa mwisho wa mwaka.


Mazao ya kwanza ya shamba yako utayaleta katika nyumba yangu mimi Yawe, Mungu wako. Usipike mwana-kondoo au mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.


Sehemu ya kwanza ya malimbuko yenu na vya matoleo yenu ya kila aina vitakuwa kwa ajili ya makuhani. Tena mutawapa sehemu ya kwanza ya unga wenu, kusudi mulete baraka juu ya nyumba zenu.


Mutakapoingia katika inchi ya Kanana ambayo ninawapa kuwa urizi wenu, nami nikifanya namna ya ukoma uote katika ukuta wa nyumba fulani katika inchi mutakayorizi,


Kuhani atafanya nayo kitambulisho cha kunitolea siku inayofuata siku ya Sabato kusudi mupate kukubaliwa.


Kila jamaa italeta mikate miwili ya sadaka ya kutoa kwa kitambulisho mbele yangu mimi Yawe. Kila mukate utatengenezwa kwa kilo mbili za unga laini uliotiwa chachu na huo mutanitolea mimi Yawe ukiwa ni matoleo ya malimbuko yenu.


Uwaambie Waisraeli kwamba mutakapofika katika inchi ninayowapa ambamo mutaishi,


Katika siku ya kwanza ya sikukuu ya majuma wakati munapomutolea Yawe malimbuko ya ngano zenu, mutafanya mukutano mutakatifu; musifanye kazi.


Donge la kwanza la unga wenye kupondwa likitolewa kwa Mungu, mikate itakuwa yake vilevile. Na kama shina la muti likitolewa kwa Mungu, matawi yatakuwa yake vilevile.


“Mutahesabu majuma saba; mutaanza kuyahesabu tangu munapoanza kuvuna ngano.


Kwa mapenzi yake mwenyewe alitupatia sisi uzima kwa njia ya ujumbe wa kweli, kusudi tupate kuwa kama mavuno ya kwanza katikati ya viumbe vyake.


Na mara tu hao waliobeba Sanduku la Agano walipofika Yordani na miguu yao ilipokanyaga kwenye ukingo wa muto ule (muto Yordani unafurika wakati wa mavuno),


Watu wale ndio waliojilinda katika usafi bila kujichafua kwa kulala na wanawake, nao wanamufuata Mwana-Kondoo kila fasi anapokwenda. Wamekombolewa kati ya watu wengine kusudi wakuwe wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo kama vile sadaka ya mavuno ya kwanza.


Hivi ndivyo Naomi pamoja na mukwe wake Ruta wa Moabu walivyorudia kutoka Moabu, na wakafika Betelehemu wakati mavuno ya shayiri yalipokuwa yanaanza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ