Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 22:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Musichafue jina langu takatifu, maana ni lazima niheshimiwe kati ya watu wa Israeli. Mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 22:32
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yawe wa majeshi anatukuzwa wakati sheria yake inafuatwa. Utakatifu wa Mungu Mutakatifu unaonyeshwa wakati haki inatendwa.


Munitambue mimi peke yangu, Yawe wa majeshi, kuwa mutakatifu. Muniogope na kuniabudu mimi peke yangu.


Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.


Usimutoe mutoto wako yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki maana kufanya hivyo utazarau jina langu mimi Mungu wako. Mimi ni Yawe.


Mushike masharti yangu na kuyatimiza. Mimi ni Yawe ninayewatakasa.


kusudi asichafue watoto wake mwenyewe. Mimi ni Yawe niliyemutakasa.


Utamutambua kuhani kuwa aliyetakaswa, maana yeye ndiye anayetolea sadaka ya mukate wa Mungu wako. Utamutambua kuwa mutakatifu, maana mimi Yawe ninayekutakasa wewe ni mutakatifu.


na hivyo kufanya watu wabebe sababu ya uovu na makosa yao kwa kula vitu vyao vitakatifu. Mimi Yawe ndiye ninayetakasa vitu hivyo.


Umwambie Haruni na wana wake makuhani waheshimu vitu ambavyo Waisraeli wametakasa kwa ajili yangu, kusudi wasichafue jina langu takatifu. Mimi ni Yawe.


Kwa hiyo mutashika na kutimiza amri zangu. Mimi ni Yawe.


Ni mimi niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi nikuwe Mungu wenu. Mimi ni Yawe.


Basi muangalie namna munavyopaswa kusema munapoomba: ‘Baba yetu unayekuwa mbinguni, Jina lako litukuzwe;


Yesu akawaambia: “Munapoomba, museme: ‘Baba! Jina lako litukuzwe; Ufalme wako ukuje.


Uwatakase wapate kujitoa kwako kabisa kwa njia ya ukweli, maana yake kwa njia ya neno lako la kweli.


Tunawaandikia ninyi kanisa la Mungu linalokuwa Korinto, ninyi ambao mumetakaswa kwa njia ya kuungana kwenu na Yesu Kristo na mumeitwa na Mungu kuwa watu wake. Vilevile barua hii ni kwa wote wanaoabudu jina la Bwana Yesu Kristo fasi zote, anayekuwa Bwana wao na Bwana wetu vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ