Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 22:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Inakatazwa kutoa chochote kinachokuwa na kilema maana hakitakubaliwa kwa faida yenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 22:20
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, mutatoa sadaka ya mwana-ngombe dume asiyekuwa na kilema kwa kutakasa hekalu langu.


Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;


Nyama ambaye kiungo chake cha uzazi kimeumizwa, kimepondwa, kimevunjwa au kimekatwa, usimutolee Yawe wala kumutoa kama vile sadaka katika inchi yako.


Wala usipokee kutoka kwa wageni nyama wa namna hiyo na kunitolea mimi Mungu wako kama chakula. Nyama hao wana kilema kwa vile wamekatwa na hawatakubaliwa kwa faida yenu.


Kama mutu anatoa sadaka ya amani na sadaka yake ni ngombe dume au dike, nyama huyo asikuwe na kilema mbele yangu.


Kama sadaka hiyo ya amani unayomutolea Yawe ni kutoka kundi la kondoo au mbuzi, basi achaguliwe dume au dike asiyekuwa na kilema.


Munaponitolea sadaka ya nyama anayekuwa kipofu, au kilema, au mugonjwa, huo si uovu? Mutawala atapendezwa au kukutendea mema ukimupa zawadi ya nyama kama yule? –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Haya ni masharti ya sheria ambayo mimi Yawe ninatoa. Uwaambie Waisraeli wawaletee ngombe dike mwekundu mukamilifu asiyekuwa na kilema chochote, na ambaye hajapata kufungwa nira.


Mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu ya kumupendeza Yawe: mwana-ngombe mumoja, kondoo dume mumoja, wana-kondoo saba wa mwaka mumoja. Wote wasikuwe na kilema.


Lakini nyama huyo akiwa na kilema chochote, ni kusema kiwete au kipofu, au ana kilema chochote kikubwa, usimutoe kuwa sadaka kwa Yawe, Mungu wako.


“Musitoe sadaka kwa Yawe, Mungu wenu, ngombe au kondoo mwenye kilema; hiyo ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


Lakini mulikombolewa kwa njia ya damu yenye bei kali ya Kristo, aliyekuwa kama kondoo asiyekuwa na kilema wala uchafu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ