Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 21:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Binti wa kuhani yeyote akijichafua kwa kufanya ukahaba, atateketezwa kwa moto maana anamuchafua baba yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 21:9
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha miezi mitatu, Yuda akapata habari hii: “Tamari, muke wa mwana wako amekuwa kahaba, tena amepata mimba kwa kufanya ukahaba.” Basi, Yuda akaamuru: “Mumutoshe inje achomwe kwa moto!”


Mutashika Sabato, nayo itakuwa kwenu siku takatifu. Yeyote atakayeichafua siku hiyo anapaswa kuuawa. Na mutu atakayefanya kazi yoyote siku hiyo atatengwa mbali na watu wake.


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Muwaue wazee palepale, vijana wanaume na wabinti, watoto na wanawake; lakini kila mumoja mwenye kuwa na kitambulisho, musimuguse. Muanzie katika hekalu langu. Basi, wakaanza na wazee waliokuwa mbele ya nyumba ya Yawe.


Usimuchafue binti yako kwa kumufanya kahaba, inchi nzima isipate kuangukia katika ukahaba na hivyo kujaa uovu.


Kama mwanaume akioa muke na vilevile kumwoa mama yake, huo ni uovu. Wote watatu wanapaswa kuteketezwa kwa moto maana wamefanya uovu. Mutafanya hivyo kwa kukomesha uovu kati yenu.


Nitawaazibu watoto wenu na ninyi wenyewe kutokana na uovu wenu, na kuzipakaa nyuso zenu mavi ya nyama wenu wa sadaka. Nitawafukuza mbali nami.


watamupeleka kwenye mulango wa nyumba ya baba yake na wanaume wa muji huo watamupiga mawe akufe, kwa sababu amefanya upumbafu katika Israeli kwa kufanya ukahaba akiwa katika nyumba ya baba yake. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.


muzee wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja nao watoto wake wanapaswa kuwa waamini na wasioshitakiwa neno juu ya mwenendo mubaya au juu ya kukosa utii.


Mutu yeyote atakayepatikana akiwa na vitu vilivyotolewa viangamizwe atateketezwa kwa moto, yeye pamoja na kila kitu chake maana ameliasi agano langu mimi Yawe, akatenda jambo la haya katika Israeli.’ ”


Yoshua akamwuliza Akana: “Kwa nini umetuletea taabu? Yawe atakuletea taabu wewe mwenyewe leo.” Waisraeli wote wakamupiga Akana kwa mawe mpaka akakufa. Kisha wakawapiga jamaa yake yote kwa mawe mpaka wakakufa, wakawateketeza wote kwa moto.


Zambi hii ya vijana hao wa Eli ilikuwa kubwa sana mbele ya Yawe. Maana, vijana hao walizarau matoleo ya Yawe.


Na litakalowapata watoto wako wawili, Hofuni na Finehasi, ni hili: Wote wawili watakufa siku moja. Hiki kitakuwa ni kitambulisho kwako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ