Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 21:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Utamutambua kuhani kuwa aliyetakaswa, maana yeye ndiye anayetolea sadaka ya mukate wa Mungu wako. Utamutambua kuwa mutakatifu, maana mimi Yawe ninayekutakasa wewe ni mutakatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 21:8
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Mungu, kumbuka jinsi watu walivyochafua ukuhani na agano la kikuhani na la Walawi.


Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa watu uwatakase leo na kesho. Uwaambie wafue nguo zao


Basi, Musa akashuka toka juu ya mulima na kuwaendea watu, akawatakasa, nao wakafua nguo zao.


Utamuvalisha ndugu yako Haruni na wana wake nguo zile, kisha uwapakae mafuta na kuwawekea mikono kwa kuwatakasa wanitumikie kama vile makuhani.


Haya ndiyo mambo utakayowafanyia Haruni na wana wake kwa kuwatakasa wapate kunitumikia kama vile makuhani. Utatwaa mwana-ngombe dume na kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema,


Uwaambie Waisraeli wote pamoja hivi: Mukuwe watakatifu maana mimi Yawe, Mungu wenu, ni mutakatifu.


Watakuwa watakatifu kwa Mungu wao wala wasichafue jina la Mungu wao. Maana wao ndio wanaotolea zile sadaka Yawe anazopewa kwa moto, ni kusema chakula cha Mungu. Basi, wanapaswa kuwa watakatifu.


na hivyo kufanya watu wabebe sababu ya uovu na makosa yao kwa kula vitu vyao vitakatifu. Mimi Yawe ndiye ninayetakasa vitu hivyo.


Kuhani ataviteketeza hivyo vyote juu ya mazabahu kama vile chakula Yawe anachotolewa kwa moto.


Munalizarau kwa kunitolea kwenye mazabahu yangu sadaka ya chakula kichafu. Lakini ninyi munauliza: Tumekichafua namna gani? Munakichafua kwa kuizarau mazabahu yangu.


Uwaamuru Waisraeli maneno haya: Ninyi mutanitolea kwa wakati wake sadaka zinazotakiwa: vyakula vya kuteketezwa kwa moto, vyenye harufu nzuri ya kupendeza.


Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?


Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ