23 Lakini asilikaribie lile pazia wala ile mazabahu maana ana kilema, asipate kuchafua Pahali Patakatifu, kwa sababu mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.
Ee Mungu, kumbuka jinsi watu walivyochafua ukuhani na agano la kikuhani na la Walawi.
Ndivyo mutakavyotenga Waisraeli na uchafu wao, kusudi wasikufe katika uchafu wao juu ya kuchafua hema langu linalokuwa kati yao.
Uwaambie Waisraeli wote pamoja hivi: Mukuwe watakatifu maana mimi Yawe, Mungu wenu, ni mutakatifu.
Kwa hiyo, mujitakase mukuwe watakatifu, maana mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Kwa sababu ametakaswa kwa kupakwa mafuta ya Mungu wake juu ya kichwa, basi asiondoke katika Pahali Patakatifu wala asipachafue. Mimi ni Yawe.
Mutu huyo anaweza kula mukate wa Mungu wake, vitu vitakatifu na vile vitakatifu kabisa.
Musa akamwelezea Haruni na wana wake na Waisraeli wote mambo hayo yote.
Watakuwa watakatifu kwa Mungu wao wala wasichafue jina la Mungu wao. Maana wao ndio wanaotolea zile sadaka Yawe anazopewa kwa moto, ni kusema chakula cha Mungu. Basi, wanapaswa kuwa watakatifu.
na hivyo kufanya watu wabebe sababu ya uovu na makosa yao kwa kula vitu vyao vitakatifu. Mimi Yawe ndiye ninayetakasa vitu hivyo.
Ninyi wapumbafu na vipofu! Ni nini inayokuwa kubwa zaidi, zahabu au hekalu linaloifanya zahabu ile ihesabiwe kuwa takatifu?