Walawi 21:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Yawe akamwambia Musa: Uwaambie makuhani, wana wa Haruni, kwamba kusikuwe mutu yeyote kati yao atakayejichafua kwa kugusa maiti ya watu wa jamaa yake,
Hawatasogelea maiti kusudi wasijichafue. Lakini wataweza kujichafua kwa kusogelea maiti ya baba au mama au mutoto wa kike au wa kiume au dada asiyeolewa.
Na hii ndiyo sheria ya kufuatwa kama mutu akikufia ndani ya hema: Kila mutu atakayeingia ndani ya hema hilo, au aliyekuwa ndani ya hema hilo, atakuwa muchafu kwa siku saba.
Mutu yeyote akigusa mwili wa mutu aliyeuawa au aliyekufa kifo cha kawaida inje ya nyumba, au akigusa mufupa wa mutu au kaburi, atakuwa muchafu kwa siku saba.