Sisi wote, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango, waimbaji, watumishi wa hekalu na watu wote waliojitenga na mataifa jirani kufuata sheria ya Mungu pamoja na wake zao, wana wao, na wabinti zao, wote wenye maarifa na ufahamu,
Maana namna gani itajulikana kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako, mimi na watu wako kama usipokwenda pamoja nasi? Ukienda pamoja nasi itatufanya mimi na watu wako kuwa watu wa pekee kati ya watu wote katika dunia.
Kwa sababu mimi ni Yawe, Mungu wenu, mujitakase na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu. Wala musijichafue na kitu chochote kinachotambaa juu ya inchi.
Mufanye hivyo kwa sababu ninyi mumetakaswa kwa Yawe, Mungu wenu. Kati ya watu wote katika ulimwengu aliwachagua ninyi kusudi mukuwe taifa lake mwenyewe.
Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.
Lakini Yoshua akawaambia: “Ninyi hamuwezi kumutumikia Yawe, maana yeye ni Mungu Mutakatifu. Yeye ni Mungu mwenye wivu, naye hatawasamehe makosa na zambi zenu.
“Umwandikie malaika wa kanisa la Filadelfia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa mutakatifu na mwenye ukweli, anayekuwa na ufunguo wa mufalme Daudi, anayefungua mulango wala hakuna anayeweza kuufunga, anayefunga wala hakuna anayeweza kuufungua.
Na kila kimoja cha viumbe vya ajabu kilikuwa na mabawa sita yenye kujaa macho ndani na inje. Navyo viliimba muchana na usiku bila kuchoka, vikisema: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwa, anayekuwa na anayekuja.”