Musifanye kama vile watu wa inchi ya Misri ambako mulikaa wanavyofanya, wala musifanye kama vile watu wa inchi ya Kanana ambako ninawapeleka wanavyofanya. Musifuate desturi zao hata kidogo.
Kwa hiyo mushike kwa ukamilifu yote ninayowaagiza. Musifuate tabia zozote ya kuchukiza zilizofanywa na wale walioishi katika inchi mbele yenu, kusudi musijichafue kwa njia yake. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.