Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 20:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu yeyote kati ya Waisraeli au mugeni anayekaa kati yenu, akimutoa mutoto wake yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki, mutu huyu anapaswa kuuawa. Wanainchi wa pale watamwua kwa kumupiga mawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 20:2
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Juu ya mulima unaokuwa upande wa mashariki wa Yerusalema, Solomono alijenga pahali pa kumutambikia Kemosi, mungu wa chukizo wa Wamoabu, na nafasi ya kumutambikia Milkomu, mungu wa chukizo wa Waamoni.


Waliwatambikia watoto wao wa kiume na wa kike kwa miungu ya uongo; wakaomba shauri kwa watabiri na wachawi. Walijitoa kabisa kutenda maovu mbele ya Yawe, wakamukasirikisha sana.


Mufalme Yosia aliharibu pahali pa kuabudia miungu ya uongo palipoitwa Tofeti katika bonde la wana wa Hinomu, kusudi mutu yeyote asimuteketeze mwana wake au binti yake kama sadaka kwa Moleki.


akafukiza ubani kwenye Bonde la mwana wa Hinomu na kuwateketeza wana wake kama sadaka, akiiga desturi za kuchukiza za watu ambao walifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.


Na aliwatoa wana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto katika bonde la mwana wa Hinomu. Alipiga ramuli, aliaguza na alitumia hirizi; hata alishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Walimwanga damu ya wasiokuwa na kosa, damu ya watoto wao wanaume na wabinti ambao waliwatoa sadaka kwa sanamu za Wakanana, nayo inchi ikachafuliwa kwa uuaji huo.


Walimujengea mungu Bali mazabahu katika bonde la Mwana wa Hinomu, kusudi wamutolee mungu Moleki wana wao na wabinti zao, ingawa sikuwaamuru wala sikufikiria kwamba wangefanya hivyo. Wakasukuma watu wa Yuda watende zambi.


Wamejenga mazabahu inayoitwa “Tofeti” huko kwenye bonde la Mwana wa Hinomu, kwa kuwatolea wana na wabinti kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Mimi sikukuwa nimewaamuru kufanya jambo hilo, wala halikunifikia katika mafikiri.


Nikawaacha wajichafue kwa sadaka zao za kuwatoa wazaliwa wao wa kwanza sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Hili lilikuwa pigo lao la azabu ya kutisha kusudi watambue kwamba mimi ni Yawe.


Munapoendelea kutoa sadaka zenu na kuwateketeza watoto wenu kwa moto munajichafua mpaka leo hii. Nitaulizwa shauri nanyi, enyi watu wa Israeli? Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– sitakubali kuulizwa shauri nanyi.


Wamefanya uzinzi na mauaji. Wamefanya ukahaba kwa sanamu zao, hata kuzitambikia watoto walionizalia wao wenyewe.


Siku ileile walipozitambikia watoto wao wenyewe kwa sanamu, waliingia Pahali Patakatifu pangu kusudi wapachafue. Hayo ndiyo waliyofanya katika nyumba yangu.


Mutu yeyote kati ya Waisraeli au mugeni anayekaa kati yao akienda kuwinda nyama au ndege, anapaswa kumwanga damu chini na kuifunika kwa udongo.


Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni, anayekula chochote kilichokufa chenyewe au kilichouawa na nyama wa pori anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi. Nyuma ya hapo atakuwa safi.


Uwaambie kwamba mutu yeyote kati ya Waisraeli au mugeni anayeishi kati yao, anayetoa sadaka ya kuteketezwa au sadaka ingine,


Usimutoe mutoto wako yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki maana kufanya hivyo utazarau jina langu mimi Mungu wako. Mimi ni Yawe.


Mwanaume au mwanamuke yeyote anayekuwa mulozi au muchawi, anapaswa kuuawa kwa kupigwa mawe. Damu yao itakuwa juu yao wenyewe.


Umuondoe kijana aliyetukana inje ya kambi, wale wote waliomusikia akitukana waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na wote pamoja wamwue kwa kumupiga mawe.


Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni anayemutukana Yawe, wote pamoja watamwua kwa kumupiga mawe.


Basi, Musa akawaambia Waisraeli hayo yote. Wakamupeleka yule mutu aliyelaani Yawe inje ya kambi, wakamwua kwa kumupiga mawe. Ndivyo Waisraeli walivyofanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Mulitembea mukibeba hema ya mungu wenu Moleki nayo sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani. Mulijitengenezea sanamu hizo kusudi muziabudu. Kwa hiyo nitawahamisha mbali kupita muji Babeli.’


Musimwabudu Yawe, Mungu wenu, hivyo, kwa maana kila chukizo ambalo Yawe hapendi, wameifanyia miungu yao, hata wamewachoma ndani ya moto watoto wao wanaume na wanawake, kwa kutambikia miungu yao.


“Kama mukisikia katika mumoja wa miji yenu kuna mwanaume au mwanamuke anayetenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wenu, na kuvunja agano lake


Kusikuwe mutu yeyote kati yenu anayemupitisha kwenye moto mutoto wake mwanaume au mwanamuke kuwa tambiko, wala mutu anayepiga ramuli, wala mwaguzi, wala mwenye kufanya uganga,


Hapo watu wa muji huo watamupiga mutoto huyo mawe mpaka akufe. Ndivyo mutakavyokomesha ubaya huo kati yenu. Kila mutu katika Israeli atasikia tukio hilo na kuogopa.


watamupeleka kwenye mulango wa nyumba ya baba yake na wanaume wa muji huo watamupiga mawe akufe, kwa sababu amefanya upumbafu katika Israeli kwa kufanya ukahaba akiwa katika nyumba ya baba yake. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ