Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Mutu yeyote akileta sadaka ya ngano kwa Yawe, sadaka hiyo ikuwe ya unga laini. Atautia mafuta na ubani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 2:1
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

mikate isiyotiwa chachu, maandazi yasiyotiwa chachu yaliyopondwa kwa mafuta, na mikate myembamba isiyotiwa chachu, lakini iliyopakwa mafuta. Vyote hivi vikuwe vimetengenezwa kwa unga laini wa ngano.


Hamujaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa sadaka zenu. Nami sikuwalemea ninyi kwa kutaka sadaka, wala sikuwachokesha kwa kuwadai ubani.


Watawarudisha wandugu zenu wote kutoka katika mataifa yote kama matoleo yangu mimi Yawe. Watawaleta juu ya farasi, juu ya nyumbu, juu ya ngamia na ndani ya magari na juu ya vipoyi mpaka Yerusalema, kwenye mulima wangu mutakatifu. Watawaleta kama Waisraeli wanavyoleta sadaka ya unga katika chombo safi mpaka ndani ya nyumba yangu mimi Yawe.


akaniambia hivi: Hapa ndipo makuhani watakapopikia nyama ya sadaka ya malipo ya kosa, sadaka ya kusamehewa zambi, na kupika sadaka za vyakula. Kwa hiyo hawatoki inje ya baraza na chochote, kusudi watu wasijichafue kwa kugusa kitu kitakatifu.


Sadaka za vyakula na za kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Yawe. Makuhani, watumishi wa Yawe, wanaomboleza.


Labda Yawe, Mungu wenu, atabadilisha nia na kuwapa baraka ya mazao, mutaweza kumutolea sadaka za chakula na kinywaji.


Siku ya nane ataleta wana-kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema, kondoo dike wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema, kilo tatu za unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula pamoja na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.


Kila mustari utautia ubani safi kusudi uambatane na mikate hiyo na kuwa sehemu ya sadaka ya kuteketezwa ya ukumbusho kwa Yawe.


Ikiwa hawezi kutoa hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kama vile sadaka yake kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi, ataleta unga kilo moja. Lakini hatautia mafuta wala ubani maana ni sadaka kwa ajili ya zambi.


Hii ndio sheria juu ya ibada inayoelekea sadaka ya vyakula. Wazao wa Haruni ndio wanaokuwa na uwezo wa kumutolea Yawe sadaka hiyo juu ya mazabahu.


Kisha akaleta mbele sadaka ya unga akijaza mukono mumoja na kuiteketeza juu ya mazabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya kila asubui.


ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja kwa ajili ya sadaka ya amani, wamutolee Yawe sadaka pamoja na sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa maana leo Yawe atawatokea.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Kati ya vitu vitakatifu kabisa ambavyo haviteketezwi kwa moto, hivi vitakuwa vyenu: sadaka za vyakula, sadaka kwa ajili ya zambi na sadaka za kosa. Kila kitu watu watakachonitolea kama vile sadaka takatifu kitakuwa chako na wana wako.


kila mumoja atatolewa pamoja na sadaka ya vyakula ya kilo moja ya unga uliochanganywa pamoja na litre moja ya mafuta bora yaliyopondwa.


Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za vinywaji pamoja na wale wana-ngombe dume, kondoo na wana-kondoo, kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.


Kisha watatwaa mwana-ngombe dume mumoja pamoja na sadaka yake ya vyakula, ni kusema unga laini uliochanganywa na mafuta; nawe utatwaa mwana-ngombe dume wingine kwa ajili ya zambi.


Yesu akawaambia: “Mimi ni mukate wa uzima. Anayenikubali hatasikia njaa hata kidogo, na yule anayeniamini hatasikia kiu hata kidogo.


Lakini munajazwa na Roho Mutakatifu ambaye Kristo alimimia juu yenu, na kwa hiyo ninyi wote munajua ukweli.


Lakini Kristo amemimia Roho juu yenu. Na kufuatana na vile Roho yule anavyokaa ndani yenu, hamuhitaji kufundishwa na mutu, kwa maana Roho wake anawafundisha mambo yote. Roho yule anasema ukweli wala hasemi uongo. Basi kama vile Roho alivyowafundisha, mukae ndani ya Kristo.


Lakini ninyi wapendwa wangu, muendelee kusimama imara katika imani yenu inayokuwa takatifu sana, mukiomba kwa uwezo wa Roho Mutakatifu.


Kisha malaika mwingine akakuja kusimama karibu na mazabahu. Alikuwa akishika chetezo cha zahabu. Naye akapewa ubani mwingi kusudi autoe sadaka pamoja na maombi ya watu wote wa Mungu juu ya mazabahu ya zahabu iliyokuwa mbele ya kiti cha kifalme.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ