Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 19:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Utakapovuna mavuno ya inchi yako, usivune kabisa mpaka kwenye mupaka wa shamba wala usirudi nyuma kukusanya mabaki.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 19:9
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Musirudie kukusanya kila kitu katika shamba la mizabibu, wala usiokote zabibu zilizoanguka chini. Utawaachia wamasikini na wageni. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Naye atakayekula nyama hiyo anapaswa kubeba lazima ya uovu wake kwa sababu amechafua kitu kitakatifu cha Yawe. Mutu huyo atatengwa na watu wake.


Uwaambie Waisraeli hivi: Mutakapoingia katika inchi ambayo ninawapa na kuvuna mazao yake, mutamuletea kuhani muganda wa mavuno ya kwanza.


Unapovuna mavuno yako katika shamba, usivune kabisa mpaka kwenye mupaka wa shamba lako wala usirudi nyuma kukusanya mabaki. Utawaachia hayo wamasikini na wageni. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Mutu yeyote asiyefunga kula siku hiyo ni lazima atengwe mbali na watu wake.


Naye Ruta alipoendelea kuokota mavuno, Boazi akawaambia watumishi wake: “Muache akusanye hata pahali miganda inapokuwa wala musimukaripie.


Siku moja, Ruta wa Moabu akamwambia Naomi: “Muniruhusu niende kukusanya masalio ya mavuno pahali nitakapopata kukubaliwa na mwenye shamba.” Naomi akamwambia: “Basi, uende binti yangu.”


Halafu Boazi akamwambia Ruta: “Sasa sikiliza binti yangu. Usiende kuokota masuke pahali pengine, lakini katika shamba hili tu. Ushikamane na wanawake hawa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ