6 Sadaka hiyo inapaswa kuliwa siku hiyohiyo inapotolewa au kesho yake. Chochote kinachobaki mpaka kwa siku ya tatu kinapaswa kuteketezwa kwa moto.
Vilevile musiache nyama yoyote mpaka asubui. Nyama yoyote itakayobaki mpaka asubui mutaiteketeza kwa moto.
Munaponitolea mimi Yawe sadaka za amani, mutanitolea kama vile inavyotakiwa kusudi mupate kukubaliwa.
Kama sehemu ya nyama yake ikikuliwa siku ya tatu, tendo hilo ni chukizo na sadaka hiyo haitakubaliwa.