Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 19:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Munaponitolea mimi Yawe sadaka za amani, mutanitolea kama vile inavyotakiwa kusudi mupate kukubaliwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 19:5
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Hezekia akawapanga tena makuhani na Walawi katika makundi, akamupa kila mumoja wao kazi kufuatana na utumishi wake katika sehemu mbalimbali za hekalu la Yawe. Kazi ile ni pamoja na utoaji wa sadaka za kuteketeza kwa moto na za amani, za shukrani na za kusifu.


Kisha akatuma vijana wa watu wa Israeli wamutolee Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na kumuchinjia sadaka za amani za ngombe.


Mufalme anapotaka kumutolea Yawe sadaka kwa mapenzi yake, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, watamufungulia mulango wa kiwanja cha ndani unaoelekea upande wa mashariki. Atatoa sadaka kama anavyofanya siku ya Sabato, na anapotoka, mulango ufungwe nyuma yake.


Tokea inje, mufalme ataingia katika baraza ya ndani kwa kupitia kwenye mulango wa baraza hiyo. Naye atasimama karibu na nguzo ya mulango, wakati makuhani wanateketeza sadaka zake za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Kisha mufalme huyo atainama chini kwenye mulango kwa kuabudu na kisha atatoka inje. Mulango utabaki wazi mpaka magaribi.


Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;


Musigeukie sanamu za miungu, wala musijitengenezee sanamu za kuyeyushwa za miungu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Sadaka hiyo inapaswa kuliwa siku hiyohiyo inapotolewa au kesho yake. Chochote kinachobaki mpaka kwa siku ya tatu kinapaswa kuteketezwa kwa moto.


kusudi apate kukubalika, atatoa katika ngombe dume au katika kondoo beberu asiyekuwa na kilema.


Mutu yeyote anapomutolea Yawe sadaka ya amani kwa kutimiza kiapo au sadaka ya mapenzi kutoka katika kundi lake la mifugo, kusudi akubaliwe anapaswa kuwa nyama mukamilifu, nyama huyo asikuwe na kilema chochote.


Ngombe dume au mwana-kondoo anayekuwa na kiungo kimoja kirefu au kifupi kuliko kawaida wanaweza kumutoa sadaka ya mapenzi. Lakini huyo usimutoe kuwa sadaka ya kutimiza kiapo.


Utakaponitolea mimi Yawe sadaka ya shukrani utaitoa kwa namna ambayo itakufanya ukubaliwe.


Lakini kama sadaka hiyo ya amani ni ya kutimiza kiapo au ya mapenzi mema, itakuliwa siku hiyohiyo inapotolewa na sehemu ingine inaweza kukuliwa kesho yake.


Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani inakuliwa kwa siku ya tatu, mutu aliyeitoa hatakubaliwa, wala hiyo sadaka haitapokelewa kwa faida yake. Nyama hiyo ni chukizo na mutu atakayeikula atabeba lazima ya uovu wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ