Wewe umetenda uovu mubaya zaidi kuliko waliotenda wale waliokutangulia. Wewe umenikasirikisha kwa kujitengenezea miungu mingine na sanamu za kufua, kisha umeniacha.
Naye akazitwaa akaziyeyusha, akatengeneza sanamu ya mwana-ngombe. Watu wakapaaza sauti wakasema: Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa katika inchi ya Misri.
Kwa sababu mimi ni Yawe, Mungu wenu, mujitakase na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu. Wala musijichafue na kitu chochote kinachotambaa juu ya inchi.
Musijitengenezee sanamu za miungu ya uongo, musishike sanamu zao za kuchongwa wala nguzo wala sanamu za mawe yaliyochongwa katika inchi yenu na kuviabudu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Sasa, mufikiri vizuri juu ya mambo yatakayotukia. Leo ni siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kenda, siku ambayo musingi wa hekalu umekamilika. Basi mufikiri vizuri:
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayefanya sanamu ya kuchonga au ya kuyeyushwa na kuisimamisha kwa siri, kitu ambacho kimetengenezwa na mikono ya fundi na ambacho ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
Muteketeze kwa moto sanamu za miungu yao. Musitamani feza wala zahabu yao, wala musiitwae na kuifanya mali yenu. Kufanya hivyo ni mutego kwenu na ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.