Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 19:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Musiwaendee waaguzi wa mizimu wala wachawi kwa kuwaomba wawaaguzie. Mukifanya hivi, mutajichafua. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 19:31
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waliwatambikia watoto wao wa kiume na wa kike kwa miungu ya uongo; wakaomba shauri kwa watabiri na wachawi. Walijitoa kabisa kutenda maovu mbele ya Yawe, wakamukasirikisha sana.


Naye alimutoa mwana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Alipiga ramuli; aliaguza akishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Tena, kusudi mufalme Yosia atimize sheria zote zilizoandikwa katika kitabu Kuhani Mukubwa Hilkia alichokipata katika nyumba ya Yawe, aliondoa wachawi, watabiri, miungu, sanamu za miungu pamoja na vyombo vingine vilivyotumika kwa kuabudu miungu ya uongo kutoka inchi ya Yuda na kutoka Yerusalema.


Saulo alikufa kwa sababu ya kutokuwa mwaminifu; hakukuwa mwaminifu maana hakutii neno la Yawe na alikwenda kwa mwaguzi kumwomba shauri,


Na aliwatoa wana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto katika bonde la mwana wa Hinomu. Alipiga ramuli, aliaguza na alitumia hirizi; hata alishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Utaangushwa mbali sana ndani ya udongo, kutoka kule mbali utatoa sauti, maneno yako yatatoka kule chini katika mavumbi, sauti yako itatoka ndani ya udongo kama ya muzimu.


Wewe umejichokesha bure na washauri wako. Basi, wajitokeze hao wenye akili wakuokoe! Wao wanagawanya mbingu sehemusehemu, wanachunguza nyota na kutabiri kila mwezi yatakayokupata.


Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima.


Musikule nyama yoyote pamoja na damu. Musifanye ulozi wala kuaguza.


Kila mumoja wenu anapaswa kuheshimu mama yake na baba yake, na kushika Sabato zangu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Mwanaume au mwanamuke yeyote anayekuwa mulozi au muchawi, anapaswa kuuawa kwa kupigwa mawe. Damu yao itakuwa juu yao wenyewe.


Hakika walimusikiliza vizuri kwa sababu aliwashangaza kwa muda wa siku nyingi kwa njia ya uchawi wake.


kutambikia sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, kasirani, mapingano, matengano, ubaguzi,


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


Wakati ule, Samweli alikuwa amekwisha kufa, na Waisraeli wote walikuwa wamekwisha kumwombolezea na kumuzika katika muji wake Rama. Saulo alikuwa amewafukuza kutoka katika inchi wenye kutabiri na wachawi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ