Nayo sanamu aliyotengeneza, akaiweka katika nyumba ya Mungu ambayo aliizungumuzia, mbele ya Daudi na mwana wake Solomono: “Katika nyumba hii na katika Yerusalema kati ya makabila kumi na mawili ya Israeli, ndipo pahali nitakapoabudiwa milele.
Hata makuhani, viongozi wa inchi ya Yuda pamoja na watu walikosa uaminifu kabisa wakiiga matendo yote ya kuchukiza ya watu wa mataifa mengine; waliichafua nyumba ya Yawe ambayo yeye mwenyewe alikuwa ameitakasa kule Yerusalema.
Fikiri mbele ya kusema, wala usikuwe mwepesi kwa kusema neno lolote mbele ya Mungu, kwa maana Mungu yuko mbinguni na wewe uko katika dunia. Kwa hiyo usiseme maneno mengi.
Muwaue wazee palepale, vijana wanaume na wabinti, watoto na wanawake; lakini kila mumoja mwenye kuwa na kitambulisho, musimuguse. Muanzie katika hekalu langu. Basi, wakaanza na wazee waliokuwa mbele ya nyumba ya Yawe.
Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.
Akamwambia: Umwambie ndugu yako Haruni asiingie katika Pahali Patakatifu nyuma ya pazia wakati usiokubaliwa. Asiingie pahali pale maana ndipo nitakapotokea katika wingu juu ya kiti cha rehema. Asipotii, atakufa.
Akawaambia: “Imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi.’ Lakini ninyi mumeigeuza kuwa nafasi ya makutano ya wanyanganyi!”
Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Nitakaa na kuishi pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
Wakati wa hukumu unakaribia. Na hukumu itaanza na watu wa Mungu. Na kama hukumu inaanzia kwetu sisi, basi mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasiotii Habari Njema ya Mungu?