Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 19:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Musikule nyama yoyote pamoja na damu. Musifanye ulozi wala kuaguza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 19:26
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waliwatambikia watoto wao wa kiume na wa kike kwa miungu ya uongo; wakaomba shauri kwa watabiri na wachawi. Walijitoa kabisa kutenda maovu mbele ya Yawe, wakamukasirikisha sana.


Na aliwatoa wana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto katika bonde la mwana wa Hinomu. Alipiga ramuli, aliaguza na alitumia hirizi; hata alishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Naye alimutoa mwana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Alipiga ramuli; aliaguza akishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Lakini muhakikishe kwamba hamukuli damu, maana damu ni uzima. Hivyo basi, musikule uzima pamoja na nyama.


Tena, musikule damu yoyote, ikuwe ya ndege au ya nyama pahali popote munapoishi.


Ndiyo maana munapaswa kufuata sharti hili siku zote na pahali popote mutakapokaa. Musikule hata kidogo mafuta wala damu.


Yawe anasema hivi: Musiige mwenendo wa mataifa mengine, wala musishangazwe na vitambulisho vya ajabu munavyoviona katika mbingu; muyaache mataifa mengine yashangazwe navyo.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Wale Wakaldea wakamujibu: Mufalme, hakuna mutu yeyote katika dunia anayeweza kutimiza mapenzi yako. Hakuna mufalme yeyote, hata akuwe mukubwa na mwenye nguvu yapata gani aliyepata kuwauliza waganga au walozi au Wakaldea jambo kama hilo.


Uasi ni sawa na zambi ya kuaguza, na kiburi ni sawa na uovu wa kuabudu sanamu. Kwa sababu umeikataa amri ya Yawe, naye amekukataa kuwa mufalme.”


Vyura wataondoka kwako, na kwenye nyumba zenu, kwa wakubwa wako na kwa watu wako. Watabaki tu katika muto Nili.”


Lakini, mufalme wa Misri akawaita wenye hekima wake na wachawi. Wale wachawi wa Misri wakafanya vile vile kwa uchawi wao.


Lakini inafaa tuwaandikie kwa kuwaambia kwamba wajitenge na vitu vilivyochafuliwa kwa kutambikia sanamu, waepuke uasherati na wasikule nyamafu wala damu.


Lakini musikule nyama wenye damu, maana uzima uko katika damu.


yeye anakunywa nacho na kukitumia kwa kuaguza? Mumekosa sana kwa kufanya hivyo!’ ”


Lakini matunda ya kuanzia mwaka wa tano hayo munaweza kuyakula na mavuno yenu yataongezeka. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Lakini musikule damu ya nyama hao; mumwange damu hiyo chini kama vile maji.


Lakini usikule damu yake; hiyo utaimwanga chini kama vile maji.


Basi walikimbilia vitu walivyoteka, wakatwaa wana-kondoo, ngombe dume na wana-ngombe, wakachinja, wakakula nyama na damu.


Watu wengine wakamwambia Saulo: “Angalia watu wanatenda zambi mbele ya Yawe kwa kula nyama yenye damu.” Saulo akawaambia watu: “Ninyi ni waasi. Muviringishe jiwe kubwa na kulileta hapa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ