Lameki akawaambia wake zake: “Ada na Sila musikie sauti yangu! Musikilize maneno ninayosema enyi wake za Lameki. Maana niliua mutu kwa sababu ya kunipiga, nilimwua kijana kwa kuniumiza.
Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Wandugu wapendwa, musilipize kisasi ninyi kwa ninyi, lakini mumwachie Mungu wakati wa kutenda kufuatana na kasirani, maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.”
maana yeye anamutumikia Mungu kwa faida yako. Lakini kama ukifanya mabaya, umwogope kwa sababu yeye yuko na uwezo kwa kuazibu. Yeye anamutumikia Mungu wa kuazibu wale wanaofanya mabaya.
Kwa hiyo amri hizi: “Usizini, usiue, usiibe, usitamani,” pamoja na zingine zote, zinafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako sawa vile unavyojipenda mwenyewe.”