Musikilize, enyi watu wa Yakobo, enyi munaojulikana kwa jina la Israeli, ninyi munaokuwa wa uzao wa Yuda. Ninyi munaapa kwa jina la Yawe, na kudai kwamba munamwabudu Mungu wa Israeli; lakini hayo si ukweli wala sawa.
Lakini muligeuka, mukachafua jina langu, wakati mulipowakamata tena watumwa na wajakazi walewale ambao mulikuwa mumewaachilia kama walivyotaka, mukawalazimisha kuwa watumwa tena.
ukiapa kwa ukweli, kwa kufuatana na sheria, na kwa haki, kwa kusema “Kama vile Yawe anavyoishi”, halafu mataifa yatapata baraka kutoka kwangu, na kutukuzwa kwa sababu yangu.
Mimi mwenyewe nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake kwa sababu alimutoa mumoja wa watoto wake sadaka kwa mungu Moleki na hivyo akachafua Pahali pangu Patakatifu na jina langu takatifu.
Yule kijana ambaye mama yake aliitwa Selemoti binti ya Dibri wa kabila la Dani, alitukana Mungu na kuzarau jina lake. Basi watu wakamupeleka kijana kwa Musa,
Kisha kuhani akiwa amevaa nguo yake ya kitani na kapitula yake ya kitani, atatwaa majivu ya ile sadaka kutoka juu ya mazabahu na kuyaweka kando ya mazabahu.
Basi, yeye akaniambia: Ndani ya kitabu hicho kumeandikwa laana ambayo inchi nzima itakayoipata. Upande mumoja imeandikwa kwamba wizi wote watafukuzwa katika inchi, na upande mwingine imeandikwa kwamba wote wenye kuapa uongo watafanyiwa vile vile.
Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.
Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.
Lakini zaidi ya yote, wandugu zangu, musiape! Musiape kwa jina la mbingu, wala kwa jina la dunia, wala kwa jina la kitu kingine chochote. Museme “Ndiyo” ikiwa munataka kusema ndiyo. Nanyi museme “Hapana” ikiwa munataka kusema hapana, kusudi musihukumiwe na Mungu.