Walawi 19:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Musirudie kukusanya kila kitu katika shamba la mizabibu, wala usiokote zabibu zilizoanguka chini. Utawaachia wamasikini na wageni. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Watabaki wachache kama vile kisha kuangusha matunda ya mizeituni: matunda mawili au matatu katika tawi la juu; mane, matano katika matawi yanayozaa sana. –Ni ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli.
Kwa sababu mimi ni Yawe, Mungu wenu, mujitakase na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu. Wala musijichafue na kitu chochote kinachotambaa juu ya inchi.
Unapovuna mavuno yako katika shamba, usivune kabisa mpaka kwenye mupaka wa shamba lako wala usirudi nyuma kukusanya mabaki. Utawaachia hayo wamasikini na wageni. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Kama wizi au wanyanganyi wangekufikia usiku, si wao wangekuiba tu vitu wanavyokuwa navyo lazima? Ikiwa wavunaji wa zabibu wangekufikia, si wangekuachia sehemu ndogo tu? Lakini wewe, waadui zako wamekuangamiza kabisa.
Ole wangu! Mimi ninakuwa kama muvunaji kisha wakati wa mavuno; hakuna tini za kwanzakwanza ninazotamani. Ni kama wakati wa kuchuma zabibu: hakuna hata fungu moja la zabibu la kula!
“Munapovuna mavuno yenu katika shamba na kusahau masuke mengine humo, musirudi kuyatwaa, lakini muwaachie wageni, wayatima na wajane, kusudi Yawe, Mungu wenu, awabariki katika kazi zenu zote.
Lakini Gideoni akawajibu: “Mambo niliyofanya mimi si kitu kabisa yakilinganishwa na yale muliyoyafanya ninyi. Walichookota watu wa Efuraimu wakati wa mavuno ni kizuri kuliko mavuno ya jamaa yangu ya Abiezeri.
Siku moja, Ruta wa Moabu akamwambia Naomi: “Muniruhusu niende kukusanya masalio ya mavuno pahali nitakapopata kukubaliwa na mwenye shamba.” Naomi akamwambia: “Basi, uende binti yangu.”