Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 18:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Munapaswa kushika masharti yangu na maagizo yangu: yule anayeyashika ataishi. Mimi ni Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 18:5
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ukawaonya kusudi warudilie Sheria yako, hata hivyo, kwa kiburi chao, wakaacha kutii amri zako. Wakaasi maagizo yako, ambayo kwa njia yake mutu akiyatii, ataishi. Wakakuwa wenye kiburi vilevile wakakuwa wagumu, na wakakataa kuwa watiifu.


alimwambia: “Mimi ni Yawe. Umwambie mufalme wa Misri maneno yote ninayokuambia.”


Kwa hiyo, uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yawe! Mimi nitawatoa katika nira mulizowekewa na Wamisri. Nitawaokoa toka utumwa wenu. Nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuwaazibu vikali Wamisri na kuwakomboa ninyi.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Niliwapa masharti yangu na kuwafundisha maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi.


Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.


Lakini hata wazao wao hao waliniasi. Hawakufuata masharti yangu, hawakushika wala kutimiza maagizo yangu ambayo mutu akiyashika, ataishi. Walizikufuru Sabato zangu. Basi nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuitimiza hasira yangu juu yao kule katika jangwa.


Mutu yeyote wa Israeli haruhusiwi kumukaribia mwanamuke wa jamaa yake wa karibu kusudi alale naye. Mimi ni Yawe.


Yawe wa majeshi alisema hivi: Mimi Yawe sibadiliki. Ni kwa sababu hii, ee ninyi wazao wa Yakobo, hamujateketezwa.


Yesu akamujibu: “Sababu gani unaniuliza juu ya jambo linalokuwa jema? Kuna mumoja tu anayekuwa mwema. Kama ukitaka kuingia pahali utakapopata uzima wa kweli, utii amri za Mungu.”


Basi Yesu akamwambia: “Umejibu vizuri. Fanya sawa vile unavyosema, nawe utaishi milele.”


Haya ndiyo mambo Musa aliyoandika juu ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya kushika Sheria: “Mutu anayetimiza maagizo ya Sheria, ataishi kwa njia yake.”


nami nikakufa. Hivi ile amri iliyopasa kuniletea uzima ikaniletea kifo.


Na tena hakuna ushirika kati ya Sheria na imani. Lakini Maandiko Matakatifu yanasema: “Yule anayeshika maagizo ya Sheria hii ataishi kwa njia hiyo.”


Mumupende Yawe, Mungu wenu. Muitii sauti yake na kuambatana naye. Kama munafanya hivyo, mutapata maisha marefu na kuishi katika inchi ambayo Yawe aliwaahidi wazee wenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwamba atawapa.”


Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.


Musa akaendelea kusema: “Mushike basi na kufuata masharti na maagizo niliyowafundisha, kusudi mupate kuishi na kurizi inchi ambayo Yawe, Mungu wa babu zenu, anawapa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ