Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 18:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Kwa hiyo mushike kwa ukamilifu yote ninayowaagiza. Musifuate tabia zozote ya kuchukiza zilizofanywa na wale walioishi katika inchi mbele yenu, kusudi musijichafue kwa njia yake. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 18:30
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kukakuwa hata ibada za uasherati katika inchi, nao walitenda matendo ya kuchukiza, sawasawa na yale matendo ya mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele ya Waisraeli.


Alitenda machukizo kwa kuabudu sanamu za miungu kama vile Waamori walivyofanya ambao zamani Yawe aliwafukuza mbele ya watu wa Israeli.


Nyuma ya mambo haya yote kutendeka, viongozi wakanifikia na kunipa habari hii: “Watu wa Israeli, makuhani na Walawi hawakujitenga na wakaaji wa inchi ambao wanatenda machukizo: Waamoni, Wamoabu na Wamisri, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wayebusi na Waamori.


Watu wote watakaofanya mambo hayo ya kuchukiza wanapaswa kutengwa mbali na watu wao.


Musifuate desturi za taifa ninalofukuza mbele yenu. Maana waliyafanya hayo yote, nami nikawachukia sana.


Kwa hiyo, makuhani washike agizo langu, kusudi wasifanye zambi na kuuawa. Mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.


“Mumupende Yawe, Mungu wenu, na kushika siku zote masharti yake, maagizo yake na amri zake.


Atakapokwisha kuyaangamiza mbele yenu, mufanye angalisho musijiingize katika mutego kwa kuyafuata. Musijisumbue kujua kitu juu ya miungu yao, mukisema: ‘Mataifa haya yaliabudu namna gani miungu yake kusudi nasi tuwaabudu vile vile?’


Musimwabudu Yawe, Mungu wenu, hivyo, kwa maana kila chukizo ambalo Yawe hapendi, wameifanyia miungu yao, hata wamewachoma ndani ya moto watoto wao wanaume na wanawake, kwa kutambikia miungu yao.


Mimi nikabeba maiti yake, nikamukatakata vipande na kuvipeleka kwa makabila yote ya Israeli, maana wamefanya jambo la kuchukiza na potovu katika Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ