Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.
Kama mutu yeyote wa jamii ya Israeli au mugeni anayeishi kati yao anakula damu yoyote, mimi nitamukasirikia mutu yule aliyekula damu na kumutenga mbali na watu wake.
Kwa hiyo mushike kwa ukamilifu yote ninayowaagiza. Musifuate tabia zozote ya kuchukiza zilizofanywa na wale walioishi katika inchi mbele yenu, kusudi musijichafue kwa njia yake. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Mutu yeyote anayegusa kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, au kitu cha mutu kinachohesabiwa kuwa kichafu, au nyama anayehesabiwa kuwa muchafu, au kitu chochote kinahesabiwa kuwa kichafu ambacho ni chukizo, akikula nyama ya sadaka ya amani Yawe aliyotolewa, mutu huyo atatengwa na watu wake.
Yawe awatenge mbali watu wanaofanya mambo hayo kutoka kati ya wazao wa Yakobo. Na wasishiriki hata kidogo katika kutoa ushuhuda na kuleta sadaka mbele ya Yawe wa majeshi.