Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 18:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Machukizo hayo yalifanywa na watu waliokaa katika inchi ya Kanana mbele yenu, nao wakachafua inchi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 18:27
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kukakuwa hata ibada za uasherati katika inchi, nao walitenda matendo ya kuchukiza, sawasawa na yale matendo ya mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele ya Waisraeli.


lakini alifuata mwenendo wa wafalme wa Israeli. Akamutambikia hata mwana wake kwa kuteketezwa kwa moto, akifuata desturi mbaya za mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.


Alitenda maovu mbele ya Yawe kwa kutenda maovu ya mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe mbele ya watu wa Israeli.


Hata makuhani, viongozi wa inchi ya Yuda pamoja na watu walikosa uaminifu kabisa wakiiga matendo yote ya kuchukiza ya watu wa mataifa mengine; waliichafua nyumba ya Yawe ambayo yeye mwenyewe alikuwa ameitakasa kule Yerusalema.


Walijivuna, wakafanya machukizo mbele yangu. Kwa hiyo niliwaangamiza mara tu nilipoyaona hayo.


Wengine wanafanya machukizo kwa kulala na wake za jirani zao. Wengine wanalala na wake za watoto wao, na wengine wanalala na wadada zao.


Yawe anasema: Nilipowakuta Waisraeli walikuwa kama zabibu katika jangwa. Nilipowaona babu zenu, walikuwa bora kama matunda ya tini za kwanza. Lakini walipofika kule Bali-Peori, wakajitolea kwa kuabudu chukizo Bali, wakakuwa chukizo kama kile walichokipenda.


Musijichafue kwa kufanya mambo hayo maana kwa sababu ya mambo hayo ninafukuza mataifa yanayokuwa mbele yenu kwa vile wao wanafanya hayo na kujichafua.


Lakini ninyi na wageni wanaokaa kati yenu munapaswa kushika masharti yangu na maagizo yangu na wala musifanye machukizo hayo.


Basi, ninyi musifanye mambo hayo, kama sivyo inchi hiyo itawatapika kama vile ilivyolitapika taifa lililokuwa mbele yenu.


kusudi wasiwafundishe desturi zao za kuchukiza ambazo wanafanyia miungu yao, nanyi mutende zambi mbele ya Yawe, Mungu wenu.


“Mwisraeli yeyote, mwanaume au mwanamuke, hatakuwa hata kidogo kahaba wa kidini.


Wote wanaofanya mambo hayo, wote wanaotenda kwa udanganyifu ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayefanya sanamu ya kuchonga au ya kuyeyushwa na kuisimamisha kwa siri, kitu ambacho kimetengenezwa na mikono ya fundi na ambacho ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ