Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 18:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Inchi yao ilichafuliwa nami nikaiazibu, nayo ikawakataa wakaaji wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 18:25
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alitenda machukizo kwa kuabudu sanamu za miungu kama vile Waamori walivyofanya ambao zamani Yawe aliwafukuza mbele ya watu wa Israeli.


ulizotupa kwa njia ya watumishi wako manabii ukisema: ‘Inchi munayoiendea na ambayo itakuwa mali yenu ni inchi chafu, yenye uchafu wa wakaaji toka inchi mbalimbali, kwa machukizo yao, wameijaza uchafu tele, kila nafasi.


Walimwanga damu ya wasiokuwa na kosa, damu ya watoto wao wanaume na wabinti ambao waliwatoa sadaka kwa sanamu za Wakanana, nayo inchi ikachafuliwa kwa uuaji huo.


kama wakivunja masharti yangu, na kuacha kutii amri zangu,


Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele.


Maana Yawe anakuja kutoka kwake juu, kutoka makao yake huko mbinguni; kuwaazibu wakaaji wa dunia kwa uovu wao. Nayo dunia haitaficha tena wale waliouawa, lakini itaufichua umwagaji wa damu wote.


Yawe anasema hivi juu ya watu hawa: Kweli wamependa sana kutangatanga, wala hawakujizuia; kwa hiyo mimi Yawe sipendezwi nao. Sasa nitayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Nitalipiza kisasi mara mbili zaidi juu ya zambi zao na makosa yao, kwa sababu wameichafua inchi yangu na mizoga ya miungu yao yenye kuchukiza, wameijaza inchi yangu na hayo machukizo yao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Niliwaleta katika inchi yenye mboleo, muyafurahie mazao yake na mema yake mengine. Lakini mulipofika tu, muliichafua inchi yangu; inchi niliyowapa ikuwe yenu, mukaifanya chukizo.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya wachungaji wanaowachunga watu wangu: Ninyi munasambaza kondoo wangu na kuwafukuza, wala hamukuwatunza. Basi, nami vilevile nitawaazibu kwa ajili ya matendo yenu maovu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mimi sitawaazibu kwa ajili ya mambo haya? Nitaachilia taifa hili bila kulilipiza kisasi? –Ni ujumbe wa Yawe.


Basi, nisiwaazibu kwa ajili ya mambo haya yote? –Ni ujumbe wa Yawe.– Nisilipize kisasi juu ya taifa kama hili?


Nitalia na kuomboleza juu ya milima; nitaomboleza juu ya mashamba ya nyama katika jangwa, kwa sababu yamekauka kabisa, hakuna mutu anayepita pahali pale. Hakusikiliki tena sauti za ngombe; ndege na nyama wamekimbia na kutoweka.


Nitakomesha furaha zake zote, sikukuu zake za mwandamo wa mwezi na za Sabato, na sikukuu zote zilizoamriwa.


Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.


Ninyi mumezama katika uovu, kama ilivyokuwa kule Gibea. Mungu atayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Lakini ninyi na wageni wanaokaa kati yenu munapaswa kushika masharti yangu na maagizo yangu na wala musifanye machukizo hayo.


Basi, ninyi musifanye mambo hayo, kama sivyo inchi hiyo itawatapika kama vile ilivyolitapika taifa lililokuwa mbele yenu.


Kwa maana tunajua kwamba mpaka sasa viumbe vyote vinaugua kwa uchungu kama mwanamuke anayesikia maumivu ya kuzaa.


Maana yeyote anayetenda mambo haya ni chukizo kwa Yawe; na kwa ajili ya mambo haya ya kuchukiza Yawe, Mungu wenu, anafukuza watu wa namna hiyo mbele yenu.


maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.


Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ