ulizotupa kwa njia ya watumishi wako manabii ukisema: ‘Inchi munayoiendea na ambayo itakuwa mali yenu ni inchi chafu, yenye uchafu wa wakaaji toka inchi mbalimbali, kwa machukizo yao, wameijaza uchafu tele, kila nafasi.
Walimwanga damu ya wasiokuwa na kosa, damu ya watoto wao wanaume na wabinti ambao waliwatoa sadaka kwa sanamu za Wakanana, nayo inchi ikachafuliwa kwa uuaji huo.
Maana Yawe anakuja kutoka kwake juu, kutoka makao yake huko mbinguni; kuwaazibu wakaaji wa dunia kwa uovu wao. Nayo dunia haitaficha tena wale waliouawa, lakini itaufichua umwagaji wa damu wote.
Yawe anasema hivi juu ya watu hawa: Kweli wamependa sana kutangatanga, wala hawakujizuia; kwa hiyo mimi Yawe sipendezwi nao. Sasa nitayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.
Nitalipiza kisasi mara mbili zaidi juu ya zambi zao na makosa yao, kwa sababu wameichafua inchi yangu na mizoga ya miungu yao yenye kuchukiza, wameijaza inchi yangu na hayo machukizo yao. –Ni ujumbe wa Yawe.
Niliwaleta katika inchi yenye mboleo, muyafurahie mazao yake na mema yake mengine. Lakini mulipofika tu, muliichafua inchi yangu; inchi niliyowapa ikuwe yenu, mukaifanya chukizo.
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya wachungaji wanaowachunga watu wangu: Ninyi munasambaza kondoo wangu na kuwafukuza, wala hamukuwatunza. Basi, nami vilevile nitawaazibu kwa ajili ya matendo yenu maovu. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Nitalia na kuomboleza juu ya milima; nitaomboleza juu ya mashamba ya nyama katika jangwa, kwa sababu yamekauka kabisa, hakuna mutu anayepita pahali pale. Hakusikiliki tena sauti za ngombe; ndege na nyama wamekimbia na kutoweka.
Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.
Maana yeyote anayetenda mambo haya ni chukizo kwa Yawe; na kwa ajili ya mambo haya ya kuchukiza Yawe, Mungu wenu, anafukuza watu wa namna hiyo mbele yenu.
maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.
Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.