Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 18:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Musijichafue kwa kufanya mambo hayo maana kwa sababu ya mambo hayo ninafukuza mataifa yanayokuwa mbele yenu kwa vile wao wanafanya hayo na kujichafua.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 18:24
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wazao wako watarudi hapa katika kizazi cha ine, kwa sababu uovu wa Waamori haujakamilika bado.”


basi, nitawahamisha watu wangu, Waisraeli, kutoka inchi hii ambayo nimewapa; vilevile na nyumba hii ambayo niliyoitakasa kwa ajili ya jina langu, nitaitupilia mbali nami, na kuifanya kitu cha kuchekelewa na kuzarauliwa kati ya watu wa mataifa yote.


Alitenda maovu mbele ya Yawe kwa kuiga mienendo miovu ya mataifa ambayo Yawe aliyafukuza wakati watu wake wa Israeli walipokuwa wanaingia.


Nyuma ya mambo haya yote kutendeka, viongozi wakanifikia na kunipa habari hii: “Watu wa Israeli, makuhani na Walawi hawakujitenga na wakaaji wa inchi ambao wanatenda machukizo: Waamoni, Wamoabu na Wamisri, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wayebusi na Waamori.


Hivyo wakajichafua kwa matendo yao, wakakosa uaminifu kwa Mungu kama wazini.


Hata hivyo, mimi niliwatuma kwenu siku zote watumishi wangu manabii nikisema: Musifanye jambo hili baya ninalolichukia!


Wewe mwanadamu! Waisraeli walipoishi katika inchi yao waliichafua kwa mienendo na matendo yao. Niliyaona matendo yao kuwa sawa na mwanamuke anayekuwa muchafu wakati wa ugonjwa wake wa mwezi.


Musifanye kama vile watu wa inchi ya Misri ambako mulikaa wanavyofanya, wala musifanye kama vile watu wa inchi ya Kanana ambako ninawapeleka wanavyofanya. Musifuate desturi zao hata kidogo.


Kwa hiyo mushike kwa ukamilifu yote ninayowaagiza. Musifuate tabia zozote ya kuchukiza zilizofanywa na wale walioishi katika inchi mbele yenu, kusudi musijichafue kwa njia yake. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Musichafue inchi ambayo munakaa ndani yake, inchi ambayo mimi ninakaa ndani yake; maana mimi Yawe ninakaa kati yenu Waisraeli.


Basi mutu akiharibu hekalu la Mungu, Mungu atamuharibu vilevile. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ndilo hekalu lake.


Musimwabudu Yawe, Mungu wenu, hivyo, kwa maana kila chukizo ambalo Yawe hapendi, wameifanyia miungu yao, hata wamewachoma ndani ya moto watoto wao wanaume na wanawake, kwa kutambikia miungu yao.


Maana yeyote anayetenda mambo haya ni chukizo kwa Yawe; na kwa ajili ya mambo haya ya kuchukiza Yawe, Mungu wenu, anafukuza watu wa namna hiyo mbele yenu.


“Yawe, Mungu wenu akiacha kuwafukuza watu hao mbele yenu, musiseme ndani ya moyo wenu kwamba: ‘Ni kwa sababu ya uhaki wetu Yawe ametuleta tuirizi inchi hii’, ambapo Yawe amewafukuza watu hawa mbele yenu kwa sababu wao ni waovu.


Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.


Tutachagua watu kumi katika kila watu mia moja wa Israeli, watu mia moja katika kila watu elfu moja, watu elfu moja katika kila watu elfu kumi. Hao watakuwa na kazi ya kuwaletea chakula wenzao watakaokuwa na kazi ya kuuazibu muji wa Gibea katika inchi ya Benjamina kwa ajili ya ubaya wao na upotovu walioufanya katika Israeli.”


Lakini watu wa muji wa Gibea wakakuja usiku wakaizunguka nyumba nilimokuwa nimelala. Wakataka kuniua, wakamutendea kwa kinguvu habara yangu mpaka akakufa.


Mimi nikabeba maiti yake, nikamukatakata vipande na kuvipeleka kwa makabila yote ya Israeli, maana wamefanya jambo la kuchukiza na potovu katika Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ