Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 18:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Usilale na muke wa mwenzako na hivyo kujichafua naye.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 18:20
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Muda wa kufunga kilio ulipokwisha, Daudi aliagiza wamulete Batiseba na kumupeleka katika nyumba yake. Batiseba akakuwa muke wa Daudi, naye akamuzalia Daudi mutoto mwanaume. Lakini jambo hilo Daudi alilofanya lilimuchukiza Yawe.


Usimutamani mwanamuke yule kwa uzuri wake, wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.


Kama mwanaume akifanya uzinzi na muke wa mwenzake, wote wawili wanapaswa kuuawa.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


akilala na mutu mwingine bila mume wake au mutu mwingine yeyote kujua; amejichafua ingawa hakuna mutu aliyeshuhudia kitendo chake kwa sababu hakukamatwa.


Wewe unayesema kwamba haifai kuzini, kwa nini unazini? Wewe unayechukia sanamu za miungu, kwa nini unaiba vitu ndani ya hekalu zao?


Ninyi munajua hakika kwamba watenda mabaya hawatapata urizi katika Ufalme wa Mungu. Musidanganyike: waasherati, wenye kuabudu sanamu, wazinzi, waasherati wa muke kwa muke na mume kwa mume,


Matendo ya kimwili yanajulikana wazi, nayo ndiyo uasherati, uchafu, kutawaliwa na tamaa za kimwili,


“Mutu akikamatwa akilala na muke wa mutu mwingine, wote wawili, mwanaume na mwanamuke, wanapaswa kuuawa. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.


“Lakini kama mwanaume amekutana na binti aliyechumbiwa akamushika kwa nguvu, basi ni huyo mwanaume tu atakayeuawa.


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ