Basi, Daudi alituma wajumbe wamulete. Basi Batiseba akakuja kwa Daudi, naye Daudi akalala naye. Kisha akarudi kwake. Mwanamuke yule alikuwa akitoka kujitakasa kisha ugonjwa wake wa mwezi.
Uwaambie watu wa Israeli hivi: Mwanamuke akipata mimba na kuzaa mutoto mwanaume, atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba sawa vile anavyokuwa kwa wakati wake wa ugonjwa wa mwezi.
Mwanamuke yeyote anapokuwa na ugonjwa wa mwezi, atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba. Mutu yeyote atakayemugusa mwanamuke yule atakuwa muchafu mpaka magaribi.
Kama mwanaume akilala na mwanamuke huyo na damu ya huyo mwanamuke ikimudondokea huyo mwanaume, basi, mwanaume huyo atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba. Kitanda chochote huyu mwanaume atakacholalia kitakuwa kichafu.
Kama mwanaume akilala na mwanamuke anayekuwa na ugonjwa wa mwezi, wote wawili wanapaswa kutengwa na watu wao; huyo mwanaume amelala na mwanamuke aliyekuwa na ugonjwa wa mwezi, na huyo mwanamuke amefunua mutiririko wa damu yake.