“Mwalimu, Musa alituamuru: ‘Mutu akiwa na ndugu yake, naye akikufa na kuacha muke wake bila mutoto, yule ndugu yake anapaswa kumwoa yule mujane na kumuzalia ndugu yake marehemu watoto.’
Ni Herode mwenyewe aliyeamuru kwamba Yoane akamatwe na kutiwa katika kifungo. Ilitokea vile kwa sababu Herode alimwoa Herodia, muke wa ndugu yake Filipo.
“Kama wandugu wanaishi pahali fulani na mumoja wao akikufa bila kuacha mutoto mwanaume, muke wa marehemu asiolewe na mutu mwingine inje ya jamaa hiyo. Yule ndugu wa marehemu anapaswa kumwoa mujane huyo.