Ninyi mutanijengea mazabahu ya udongo. Juu yake mutanitolea kondoo wenu na ngombe wenu kama sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Pahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, pale pale mimi mwenyewe nitawafikia na kuwabariki.
Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;
bila kumuleta nyama huyo kwenye mulango wa hema la mukutano kwa kumutolea Yawe mbele ya makao yake, mutu yule atakuwa na kosa ya kumwanga damu. Amemwanga damu na atatengwa na watu wake.