Kisha Daudi akamujengea Yawe mazabahu pahali pale na kumutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Basi, Yawe akayakubali maombi kwa ajili ya inchi, na ule ugonjwa mukali uliowapata Waisraeli ikakoma.
Kama mutu yeyote wa jamii ya Israeli au mugeni anayeishi kati yao anakula damu yoyote, mimi nitamukasirikia mutu yule aliyekula damu na kumutenga mbali na watu wake.
bila kumuleta nyama huyo kwenye mulango wa hema la mukutano kwa kumutolea Yawe mbele ya makao yake, mutu yule atakuwa na kosa ya kumwanga damu. Amemwanga damu na atatengwa na watu wake.
Kwa hiyo Waisraeli watakoma kabisa kuwatambikia miungu ya uongo wenye umbo la beberu, jambo ambalo limewafanya wakose uaminifu kwangu. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyao vyote.
Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.
Basi, habari zikawafikia watu wa makabila mengine ya Israeli kwamba makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase yalikuwa yamejenga mazabahu kubwa karibu na muto Yordani katika inchi ya Kanana, ni kusema ndani ya eneo lao.
Halafu, unijengee mimi Yawe, Mungu wako, mazabahu nzuri juu ya mwinuko ule. Kisha unitolee sadaka ya kuteketezwa ya yule ngombe dume wa pili ukitumia kuni za ile sanamu ya Ashera uliyoivunja.”
Utanitangulia kwenda Gilgali, pahali ambapo nitakukuta na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani. Utaningojea pale kwa muda wa siku saba mpaka nikuje na kukuonyesha la kufanya.”
Samweli akasema: “Nitaweza kwenda namna gani? Kama Saulo akisikia habari hiyo, ataniua!” Yawe akamwambia: “Twaa mwana-ngombe pamoja nawe, na ukifika kule useme: ‘Nimekuja kumutolea Yawe sadaka’.
Kwa hiyo Samweli alitwaa mwana-kondoo anayenyonya akamutolea Yawe kama sadaka ya kuteketezwa. Kisha Samweli akamulilia Yawe kwa ajili ya Waisraeli, naye akajibu kilio chake.