Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 17:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni, anayekula chochote kilichokufa chenyewe au kilichouawa na nyama wa pori anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi. Nyuma ya hapo atakuwa safi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 17:15
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninyi mutakuwa watu waliotakaswa kwa ajili yangu. Kwa hiyo hamutakula nyama ya nyama aliyeuawa na nyama wa pori. Nyama hiyo mutaitupia imbwa.


Halafu nikamwambia hivi: Ee, Bwana wangu Yawe, sijajichafua hata kidogo kwa kula nyamafu wala nyama aliyeuawa na nyama wa pori, wala sijapata kuonja nyama anayehesabiwa kuwa muchafu tangu ujana wangu.


Makuhani hawatakula nyamafu au ndege yeyote aliyekufa mwenyewe au aliyeraruliwa na nyama wa pori.


Kugusa nyama fulanifulani kunamufanya mutu kuwa muchafu. Yeyote atakayegusa mizoga yao atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu akitwaa sehemu ya mizoga yake atakuwa muchafu mpaka magaribi na nguo zake zinapaswa kufuliwa.


Nyama wote wanaotembelea kwa vitanga vyao ingawa wana miguu mine, ni wachafu kwenu na yeyote atakayegusa muzoga wa nyama kama huyo atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote anayebeba muzoga atakuwa muchafu mpaka magaribi, naye atasafisha nguo zake. Hao ni wachafu kwenu.


Hao wote ni wachafu kwenu na yeyote atakayegusa mizoga yao, atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Ikiwa muzoga wa viumbe hao unaangukia kitu chochote, kikuwe ni kifaa cha mbao au nguo au ngozi au gunia au chombo chochote kinachotumiwa kwa kazi yoyote, chombo hicho kitakuwa kichafu mpaka magaribi. Kwa kukifanya kikuwe safi kinapaswa kusafishwa kwa maji.


Ikiwa nyama yeyote munayeruhusiwa kula, anakufa mwenyewe, yeyote atakayegusa muzoga wake, atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote akikula nyama ya muzoga huo atafua nguo yake na atakuwa muchafu mpaka magaribi. Na yeyote atakayebeba muzoga huo, atafua nguo zake, naye atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayegusa kitu chochote mutu huyu alichoikalia atakuwa muchafu mpaka magaribi. Mutu yeyote anayebeba kitu chochote kilichokuwa cha mutu huyu anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayegusa kitanda cha huyo mwanamuke anapaswa kufua nguo zake na kuoga kwa maji. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote atakayegusa kitanda cha mutu yule anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Kuhani asikule nyama yoyote ya nyama aliyekufa peke yake au kuuawa na nyama wa pori, kusudi asijichafue. Mimi ni Yawe.


Mafuta ya nyama yoyote aliyekufa mwenyewe au ya nyama aliyeuawa na nyama wa pori yanaweza kuwekwa kwa matumizi mengine, lakini musiyakule.


Katika siku ya tatu na ya saba, mutu anayekuwa safi atamunyunyizia mutu anayekuwa muchafu maji hayo; hivyo katika siku ya saba, atamutakasa mutu huyo anayekuwa muchafu, naye atafua nguo zake na kuoga, na magaribi atakuwa safi.


Hili ni sharti la kufuata siku zote. Mutu atakayenyunyiza maji ya utakaso atafua nguo zake; naye atakayegusa maji hayo atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu atakayemuteketeza ngombe huyo vilevile atafua nguo zake na kuoga mwili, lakini naye vilevile atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Musikule nyamafu yeyote lakini munaweza kumupa mugeni anayeishi katika miji yenu, akule, au munaweza kumwuzishia mutu wa taifa lingine. Musipike mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake. “Ninyi ni watakatifu na Yawe ni Mungu wenu.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ