Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 17:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kama mutu yeyote wa jamii ya Israeli au mugeni anayeishi kati yao anakula damu yoyote, mimi nitamukasirikia mutu yule aliyekula damu na kumutenga mbali na watu wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 17:10
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini musikule nyama wenye damu, maana uzima uko katika damu.


akisema: “Sina haki hata kidogo ya kunywa maji haya, ee Yawe. Maji haya si ni kama damu ya wale walioyahatarisha maisha yao kwa kuyaleta?” Kwa hiyo, Daudi hakuyakunywa maji hayo. Hayo ndiyo mambo waliyotenda wale mashujaa watatu.


Yawe anawaangalia watu wa haki, na kusikiliza malalamiko yao;


Yeyote atakayetengeneza mafuta kama haya, au kumupakaa mutu asiyestahili kupakwa mafuta haya, mutu huyu atatengwa mbali na watu wake.


Nimeamua kuleta hasara juu ya muji huu wala siyo mema. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitautoa katika mikono ya mufalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Basi, nitawageukia na kuwaletea hasara na kuiangamiza Yuda yote.


Nitapingana naye. Nitamufanya kuwa kitambulisho na mufano; nitamwondoa kabisa kutoka taifa langu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitawaazibu vikali. Hata kama wataukimbia moto, huo moto utawateketeza. Hapo nitakapowaazibu vikali, halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Basi, uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninyi munakula nyama yenye damu, munaziabudu sanamu za miungu yenu na kumwanga damu! Munazani kwamba mutapewa inchi hii ikuwe yenu?


Mumelichafua hekalu langu kwa kuruhusu waingie humo watu wasiotahiriwa, watu wasionitii mimi, wakati mafuta na damu vinatolewa kwa ajili yangu. Hivyo, ninyi watu wangu mumelivunja agano langu kwa machukizo yenu yote.


Itakuwa hivyo kwa sababu uzima wa kiumbe uko katika damu. Nimewaagiza kutolea damu kwenye mazabahu kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya roho zenu, kwa sababu damu inafanya upatanisho, nao uzima uko katika damu.


Musikule nyama yoyote pamoja na damu. Musifanye ulozi wala kuaguza.


Mimi nitawashambulia, nanyi mutapigwa na waadui zenu. Mutatawaliwa na wale wanaowachukia. Mutatishwa na kukimbia hata kama hakuna mutu yeyote anayewafukuza.


Ndiyo maana munapaswa kufuata sharti hili siku zote na pahali popote mutakapokaa. Musikule hata kidogo mafuta wala damu.


Hata wakikamatwa mateka na waadui zao, nitatoa amri kule wauawe kwa upanga. Nitawachunga kwa uangalifu sana nipate kuwatendea mabaya na si mema.


Lakini inafaa tuwaandikie kwa kuwaambia kwamba wajitenge na vitu vilivyochafuliwa kwa kutambikia sanamu, waepuke uasherati na wasikule nyamafu wala damu.


musikule vyakula vilivyotolewa kwa kutambikia sanamu; musikule damu wala nyamafu; na muepuke uasherati. Mutafanya vema kama mukijitenga na mambo haya. Salamu kwenu.”


Lakini musikule damu ya nyama hao; mumwange damu hiyo chini kama vile maji.


Lakini muhakikishe kwamba hamukuli damu, maana damu ni uzima. Hivyo basi, musikule uzima pamoja na nyama.


Lakini usikule damu yake; hiyo utaimwanga chini kama vile maji.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Basi walikimbilia vitu walivyoteka, wakatwaa wana-kondoo, ngombe dume na wana-ngombe, wakachinja, wakakula nyama na damu.


Watu wengine wakamwambia Saulo: “Angalia watu wanatenda zambi mbele ya Yawe kwa kula nyama yenye damu.” Saulo akawaambia watu: “Ninyi ni waasi. Muviringishe jiwe kubwa na kulileta hapa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ