Wakaleta ngombe dume saba, kondoo dume saba, wana-kondoo saba na mbuzi dume saba, kuwa sadaka ya maondoleo ya zambi, kwa ajili ya jamaa ya kifalme, ya Pahali Patakatifu na ya watu wa Yuda. Kwa hiyo, mufalme akawaambia makuhani waliokuwa wazao wa Haruni wawateketeze juu ya mazabahu ya Yawe.
Wakati wa kuizindua nyumba ya Mungu, walitoa ngombe dume mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia ine na beberu kumi na wawili kwa ajili ya sadaka ya kusamehewa zambi, mbuzi mumoja kwa kila kabila la Israeli.
Ikiwa kuhani ambaye amepakwa mafuta ndiye aliyetenda zambi hata akawatia watu katika kosa, basi huyo atamutolea Yawe ngombe dume muchanga asiyekuwa na kilema akuwe sadaka kwa ajili ya zambi.
Utwae Haruni na wana wake na zile nguo takatifu, mafuta ya kupakaa, ngombe wa sadaka kwa ajili ya zambi, kondoo dume wawili, na kitunga cha mikate isiyotiwa chachu.
Musa akamwambia Haruni: Twaa mwana-ngombe dume kwa ajili ya sadaka ya kuondoa zambi na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, nyama wote wasikuwe na kilema. Kisha uwatoe sadaka mbele ya Yawe.
Mutatoa vilevile beberu mumoja kwa sadaka kwa ajili ya zambi zaidi ya sadaka ya kufanyiwa upatanisho, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji.
Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.